Nishaurini: Nimegundua Pesa Ninazompa Anahonga Mwanaume Mwingine
Mimi ni kijana wa kiume nna miaka 27, kuna msichana nimekutana nae miezi minne iliopita, kiukweli ni mzuri sana pia ni mwanachuo hapa Dar, kiukweli nimemuhudia sana ndani ya miezi hiyo minne.
Nimemnunulia hadi kiwanja Chanika, simu nzuri, pesa za matumizi nampa nyingi tuu nimemwambia boom lake awasaidie wazazi nyumbani kwani aliniambia wako vibaya sana (maskini wa kutupwa)
Sasa juzi nimegundua kumbe pesa ninazompa ana kamwanamme kake nae anakahonga anasoma nako chuo.
Gharama nilizomgharamia nimecalculate ni zaidi ya M8, nikimuulza analeta kiburi anadai kama vipi tuachane.
Je, nifanyaje? Juzi washikaji zangu wamenishauri tuwateke wote tukawatese nje ya mji ikiwezekana tumuue huyo jamaa.
Mnanishauri nini?
Inauma sana
NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
Previous article
Leave Comments
Post a Comment