Monday, 17 March

Ads Right Header

Buy template blogger

Mbowe aendelea kupatiwa matibabu baada ya kuvamiwa na kujeruhiwa



Mwenyekiti Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya DCMC Ntyuka iliyopo mkoani Dodoma baada ya kuvamiwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo.

Habari kutoka jijini Dodoma zinaeleza kuwa Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, amepata majeraha kadhaa ikiwa ni pamoja kuvunjika mguu.

Baadhi ya viongozi wamefika hospitalini hapo ili kumjulia hali Mwenyekiti huyo wa CHADEMA, akiwemo Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson.

  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4