Naibu waziri wa kilimo Omar Mgumba,aagiza kukusanywa tani elfu thelathini za mazao
Na Amiri Kilagalila,Njombe
Wakala wa taifa wa hifadhi ya chakula kanda ya Makambako,mkoani Njombe umetakiwa kukusanya tani elfu thelethini za mazao kwa mwaka wa fedha wa 2020 /2021.
Agizo hilo limetolewa na Naibu waziri wa kilimo nchini Omar Mgumba wakati akizungumza na watumishi wa hifadhi hiyo,ambapo amesema kuwa lengo la serikali kitaifa ni kununua na kuhifadhi mazao tani laki tatu kwa mwaka na kanda ya Makambako inatakiwa kununua tani elfu thelathini na kuhakikisha inapata faida katika mazao hayo.
“Malengo yetu ni kuhifadhi tani laki tatu mwaka huu nikwasababu uwezo wetu kama NFRA ni kuhifadhi tani laki mbili na hamsini na moja kwa sasa,lakini kwa ujenzi huu wa vihenge Makambako niliokuja kuukagua utaongeza tani laki mbili na hamsini zingine,Kwa hiyo hapa Makambako tumewapa tani elfu thelathini lakini hatujawapa ukomo”alisema Mgumba
Aidha Naibu waziri Mgumba amewahakikishia uwepo wa soko la uhakika wakulima wa zao la Mahindi na Mpunga na kuwataka wasiuze mazao yote kwa sasa kwa kuwa uhitaji wa mazao hayo ya chakula ni mkubwa hasa nje ya nchi kutokana na mataifa mengi kukumbwa na janga la nzige na mafuriko.
Hata hivyo kaimu meneja wa wakala wa hifadhi ya chakula kanda ya Makambako Frank Felix amesema kuwa tani hizo elfu thelathini zitakusanywa kwa wakati na kueleza kuwa changamoto kubwa kwa sasa ni wananchi ambao wamekua wakipeleka mahindi ambayo hayana ubora.
“Sasa hivi tunanunua mahindi na mpunga na tayari tumeshaaanza manunuzi ya mpunga katika kituo cha Utulo ,Mbeya kwa hiyo hizo tani thelathini ni za mahindi na mpunga,wito wangu kwa wananchi wachangmkie hili soko”Alisema Frank Felix
Wakala wa hifadhi ya chakula kanda ya Makambako inanunua mahindi kwa kilo moja shilingi mia tano na hamsini na mpunga shilingi mia saba kwa kilo moja.
Wakala wa taifa wa hifadhi ya chakula kanda ya Makambako,mkoani Njombe umetakiwa kukusanya tani elfu thelethini za mazao kwa mwaka wa fedha wa 2020 /2021.
Agizo hilo limetolewa na Naibu waziri wa kilimo nchini Omar Mgumba wakati akizungumza na watumishi wa hifadhi hiyo,ambapo amesema kuwa lengo la serikali kitaifa ni kununua na kuhifadhi mazao tani laki tatu kwa mwaka na kanda ya Makambako inatakiwa kununua tani elfu thelathini na kuhakikisha inapata faida katika mazao hayo.
“Malengo yetu ni kuhifadhi tani laki tatu mwaka huu nikwasababu uwezo wetu kama NFRA ni kuhifadhi tani laki mbili na hamsini na moja kwa sasa,lakini kwa ujenzi huu wa vihenge Makambako niliokuja kuukagua utaongeza tani laki mbili na hamsini zingine,Kwa hiyo hapa Makambako tumewapa tani elfu thelathini lakini hatujawapa ukomo”alisema Mgumba
Aidha Naibu waziri Mgumba amewahakikishia uwepo wa soko la uhakika wakulima wa zao la Mahindi na Mpunga na kuwataka wasiuze mazao yote kwa sasa kwa kuwa uhitaji wa mazao hayo ya chakula ni mkubwa hasa nje ya nchi kutokana na mataifa mengi kukumbwa na janga la nzige na mafuriko.
Hata hivyo kaimu meneja wa wakala wa hifadhi ya chakula kanda ya Makambako Frank Felix amesema kuwa tani hizo elfu thelathini zitakusanywa kwa wakati na kueleza kuwa changamoto kubwa kwa sasa ni wananchi ambao wamekua wakipeleka mahindi ambayo hayana ubora.
“Sasa hivi tunanunua mahindi na mpunga na tayari tumeshaaanza manunuzi ya mpunga katika kituo cha Utulo ,Mbeya kwa hiyo hizo tani thelathini ni za mahindi na mpunga,wito wangu kwa wananchi wachangmkie hili soko”Alisema Frank Felix
Wakala wa hifadhi ya chakula kanda ya Makambako inanunua mahindi kwa kilo moja shilingi mia tano na hamsini na mpunga shilingi mia saba kwa kilo moja.
Leave Comments
Post a Comment