Rais Magufuli awashukuru Viongozi wa Dini na Watanzania wote kwa kuomba dhidi ya Corona
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza wakati alipokuwa akiendesha Harambee ya Papo kwa papo kwa ajili ya upanuzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Bikira Maria Imaculata Chamwino Ikulu mkoani Dodoma leo tarehe 7 Juni 2020. Katika Harambee hiyo jumla ya Shilingi Milioni 17 zilipatikana pamoja na mifuko 76 ya Saruji na Mhe. Rais Magufuli alichanga peke yake kiasi cha Shilingi Milioni 10.
Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Bikira Maria Imaculata Chamwino Paulo Mapalala akishukuru mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuendesha Harambee iliyofanikisha kupatikana kiasi cha ya Shilingi Milioni 17 pamoja na mifuko 76 ya Saruji.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na watumishi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Bikira Maria Imaculata Chamwino Ikulu mara baada ya Misa ya Jumapili ya Sikukuu ya Utatu Mtakatifu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Bikira Maria Imaculata Chamwino Paulo Mapalala mara baada ya misa ya Jumapili ya Sikukuu ya Utatu Mtakatifu katika Kanisa hilo. PICHA NA IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amejumuika na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Bikira Maria Imaculata Chamwino katika Misa ya Jumapili ya Sikukuu ya Utatu Mtakatifu leo tarehe 7 Juni 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Bikira Maria Imaculata Chamwino Ikulu mkoani Dodoma leo tarehe 7 Juni 2020
Previous article
Next article
Leave Comments
Post a Comment