Ads Right Header

Buy template blogger

PROFESA IBRAHIMU LIPUMBA AMSIMAMISHA NAIBU KATIBU MKUU ZANZIBAR

PROFESA IBRAHIMU LIPUMBA AMSIMAMISHA NAIBU KATIBU MKUU ZANZIBAR
Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi( CUF)Profesa Ibrahim Lipumba kwa kutumia Mamlaka ya Kikatiba,  amemsimamisha Naibu Katibu Mkuu Zanzibar  Faki Suleiman Khatib.

Taarifa ya CUF kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Julai 4,2020 imesema hatua hiyo ni katika kutekeleza agizo la Baraza Kuu la kuondoa Mapungufu na Kuimarisha Kamati Tendaji.

Hivyo nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Zanzibar itajazwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa linalotarajiwa kuketi mwishoni mwa mwezi huu.

Aidha Mwenyekiti amemteua  Nadhira Ali Haji kuwa Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Katibu Mkuu wa Chama, Haroub Mohammed Shamis.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo Prof.Lipumba ameyafanya hayo asubuhi ya leo huko Zanzibar akiwa kwenye ziara fupi ya kumtambulisha Katibu Mkuu Mpya na kushughulikia Maagizo aliyopewa na Baraza Kuu lililoketi wiki iliyopita Ukumbi wa Shaaban Khamis Mloo, Dar es Salaam.

Previous article
Next article

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4