SENZO WA SIMBA APEWA MASUALA YA LA LIGA YANGA
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, leo Agosti 24, makao makuu ya Yanga, Mwenyekiti wa timu hiyo, Mshindo Msolla amesema kuwa wanaamini wapo na mtu sahihi katika masuala ya ushauri ndani ya klabu hiyo.
"Tupo kwenye mabadiliko ambayo tayari tumeshaanza tukishirikiana na watu wa La Liga hivyo kikubwa ambacho tunakifanya ni kuwa na watu sahihi ambao watatupeleka kwenye mafanikio.
"Kwa sasa tunafanya kazi pia na Senzo ambaye ana uwezo mkubwa kwenye masuala ya michezo, tayari kwenye vikao vyetu vya La Liga ameanza kutoa mchango wake hivyo tua amini tupo na mtu sahihi," amesema.
Senzo amesema:"Nitafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na viongozi wa Yanga ikiwa ni pamoja na mwenyekiti pamoja na viongozi wengine wote kwa kuwa ninatambua majukumu yangu na kazi yangu pia.
"Kikubwa ni kusimama katika ukweli na uwazi ili kufikia malengo ambayo tumejiwekea," amesema.
Agosti 9, Yanga ilimalizana na Senzo Mbathha muda mfupi baada ya kutangaza kujiuzulu ndani ya Simba
Leave Comments
Post a Comment