Friday, 21 March

Ads Right Header

Buy template blogger

MANCHESTER UNITED WASITISHA MAZUNGUMZO YA KUIPATA SAINI YA NAHODHA WA MBWANA

MANCHESTER UNITED WASITISHA MAZUNGUMZO YA KUIPATA SAINI YA NAHODHA WA MBWANA

 


MANCHESTER United inayonolewa na Kocha Mkuu, Ole Gunnar Solskjaer imesimamisha mazungumzo ya kumpata kiungo wa Aston Villa, Jack Grealish na kumgeukia Donny van de Beek anayekipiga Ajax.


Awali ilielezwa kuwa United walikuwa wanataka saini ya nahodha huyo wa Aston Villa anakokipiga mzawa Mbwana Samatta lakini Solskjaer amesema kuwa anataka kumtazama yule wa Ajax.


United ilikuwa tayari kuweka mezani kitita cha pauni milioni 80 kupata saini yake. Kiungo huyo aliweza kuonyesha kiwango kikubwa msimu uliopita na alikiongoza kikosi chake kujinusuru kushuka daraja.


Pia mabosi wa United walikuwa wanahitaji saini ya Jadon Sancho wa Borussia Dortmund huko dili lilikuwa gumu kwa sababu ya dau walilotajiwa kuwa kubwa.

Previous article
Next article

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4