Tuesday, 18 March

Ads Right Header

Buy template blogger

JINSI YA KUEPUKA MANENO YENYE KUUMIZA


Hurtful Love | Teen Ink



NDOA❤️


👇KIKWAZO👇
Kila mara mnapobishana, MUME/MKE wako mnatupiana maneno yenye kuchambuana. Maneno yenye kuumiza yamekuwa ya kawaida katika ndoa yenu hivi kwamba sasa mmezoea kuwasiliana kwa njia hiyo👉🙄🙄🙄👈
👇
Ikiwa ndoa yako iko hivyo, unaweza kuzuia hali hiyo isiendelee. Lakini, kwanza, unahitaji kuchunguza ni nini kinachosababisha tatizo hilo na kwa nini kufanya mabadiliko kutakuwa na manufaa kwenu.🙏
👇
KWA NINI HILI HUTUKIA✔️

Malezi. Waume na Wake wengi walilelewa katika familia ambamo watu walizoea kutumiana maneno yenye kuumiza. Huenda MUME/MKE mmoja au wote wawili wakawa wanatumia maneno ambayo waliwasikia wazazi wao wakitumia.
👇
Uvutano mbaya wa burudani. Waigizaji wa filamu na televisheni hugeuza maneno ya kifidhuli kuwa jambo la kuchekesha, na hivyo kuwafanya watazamaji waone kuwa si vibaya kutumia maneno hayo.🙄🙄🙄🙄👈
👇
Utamaduni. Jamii fulani hufundisha kwamba “Wanaume halisi” huwakandamiza wengine na kwamba Wanawake wanahitaji kuwa wakali sana ili wasionwe kuwa dhaifu. Mabishano yanapotokea, huenda wenzi wa ndoa walio na mitazamo kama hiyo wakawaona wenzi wao kuwa maadui badala ya marafiki na huenda wakatumia maneno yenye kuumiza badala ya maneno yenye kuponya.
👇
Hata sababu iwe nini, maneno yenye kuumiza yanaweza kuongoza kwenye talaka na pia yanaweza kusababisha matatizo fulani ya afya. Hata wengine wanasema kwamba maneno yanaweza kuumiza zaidi kuliko kupigwa. Kwa mfano, Mwanamke mmoja ambaye Mume wake alikuwa na Mazoea ya kumpiga na kumtukana anasema hivi: “Ilikuwa vigumu zaidi kuvumilia matusi kuliko kupigwa. Afadhali angenipiga kuliko kuniambia maneno yenye kuumiza.”
👇
Mnaweza kufanya nini ikiwa uhusiano wenu umeharibika kwa sababu ya kutumia maneno yenye kuumiza❓


 MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA✔️
Onyesha hisia-MUME/MKE👇
 Jiweke katika hali ya MUME/MKE wako, na ujaribu kuelewa jinsi maneno yako yanavyofanya ahisi. Ikiwezekana, fikiria pindi hususabi ambapo MUME/MKE wako alihisi kuwa maneno uliyosema yalimuumiza. Usikazie fikira maneno uliyosema; jambo muhimu ni jinsi MUME/MKE wako anavyohisi kuhusu yale uliyosema. Je, unaweza kufikiria maneno yenye fadhili ambayo ungetumia badala ya maneno hayo yenye kuumiza❓👈Biblia inasema: “Jibu, linapokuwa la upole, hugeuza ghadhabu, lakini neno linaloumiza hufanya hasira ipande.”—Methali 15:1.
👇
Jifunze kutoka kwa wenzi wa ndoa wanaoheshimiana. Ikiwa uliiga mifano mibaya ya watu waliotumia maneno yenye kuumiza, tafuta mifano mizuri ya kuiga. Wasikilize wenzi wa ndoa ambao wanastahili kuigwa kwa sababu ya usemi wao.— Biblia: yasema katika Wafilipi 3:17. "Ndugu zangu,mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi."
👇
Amsha hisia mlizokuwa nazo. Mara nyingi maneno yenye kuumiza ni tatizo linaloanzia moyoni si kinywani. Kwa hiyo, jitahidi kuwa na hisia na mawazo yanayofaa kumhusu MUME/MKE wako. Zungumzieni mambo mliyofurahia zamani mkiwa pamoja. Angalieni picha zenu za zamani. Ni nini kilichowafanya mcheke❓ Ni sifa gani zilizomfanya kila mmoja wenu avutiwe na mwenzake❓— Biblia:yasema katika Luka 6:45."Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoka yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoka yaliyo maovu; kwa kuwa mtu ,kinywa chake hunena yale yaujazao moyo wake."
👇
Tumia neno “mimi.” Badala ya kumshambulia MUME/MKE wako kwa maneno, mweleze jinsi mambo mbalimbali yanavyokuathiri. Kwa mfano, ni rahisi kwa MUME/MKE wako kukujibu kwa maneno mazuri ukimwambia, “Mimi huhisi kuwa nimepuuzwa unapofanya mambo bila kuomba maoni yangu” badala ya kusema, “Hiyo ni kawaida yako—kila wakati unafanya mambo bila kuomba maoni yangu!”— Biblia: yasema Wakolosai 4:6."Maneno yenu yawe na neema siku zote; yakikolea munyu,mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu "
👇
Jua wakati wa kunyamaza. Ikiwa hasira inaanza kupanda na mnashindwa kudhibiti maneno yenu, lingekuwa jambo bora kuahirisha mazungumzo. Kwa kweli, hakuna ubaya wowote kuondoka mabishano yanapokuwa makali na kusubiri hadi mtakapoweza kuzungumza kwa utulivu zaidi.— Biblia: yasema katika Methali 17:14."Mwanzo wa ugomvi ni kama kutoboa penye maji; Basi acheni ugomvi kabla haujafurika "
👇
Mara nyingi maneno yenye kuumiza ni tatizo linaloanzia moyoni si kinywani
👇
NENO LA MUNGU LINASEMA👇
“Waume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.”—Waefeso 5:28.
“Mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.”—Waefeso 5:33.
“Kupiga kelele na matukano na viondolewe mbali kutoka kwenu.”—Waefeso 4:31.
“MATUKANO” NI NINI?
Biblia inasema: “Kupiga kelele na matukano na viondolewe mbali kutoka kwenu.” (Waefeso 4:31) Kwa nini Paulo alitofautisha “kupiga kelele” na “matukano”? Neno la awali lililotafsiriwa“kupiga kelele” (Kigiriki, krau·ge′) hurejelea kupaaza sauti. Kinyume na hilo, “matukano” (Kigiriki, bla·sphe·mi′a) hufafanua maana ya ujumbe unaopitishwa. Hilo linamaanisha nini?❓Matukano hayahusishi tu kupaaza sauti. Kwa kweli, usemi wowote unaokusudiwa kudhuru au wenye kushusha heshima, ni matukano—hata kama unasemwa kwa sauti ya chini.
 
 

  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4