Ads Right Header

Buy template blogger

SEPTEMBER 1 SEHEMU YA NANE.


A Walk to Remember – Movie Recommendation | Bullies2Buddies
TULIPOISHIA JANA SEHEMU YA SABA.

  "Hakuna shaka ilimradi ulinzi  uwepo, jeshi la polisi watahusika katikati ya  mabehewa tu kwa kujichanganya na raia. Askari kanzu watawekwa humo, ili usalama wa raia uwepo. Safari hii nahitaji iwe ya kihistoria, iende na kumalizika kwa usalama mkubwa bila ya kukumbwa na lolote"
TIRIRKA NA SEHEMU YA NANE ..

**
 
       Norbert  alipokaribia kufika kufika kwenye  kiwanda cha kutengeneza magari ya kuchezea watoto, aliegesha gari lake njiani kisha akashuka akiwa na mkoba mdogo. Haraka alitembea na kuingia kwenye vyoo vya  ghorofa moja lenye maduka mengi ya nguo. Huko ndani alibadili  nguo zake, alipotoka alivaa nguo ya wafanyakazi wa kiwanda   yenye rangi ya bluu pamoja na kofia   ambayo ina nembo ya mahali anapoenda
        Alirejea garini  na kuweka  mfuko ule aliyotoka nao, ambao ulihifadhi mavazi aliyoyavua. Hatimaye alitembea kwa mwendo wa  taratibu kuelekea kiwandani, alipokuwa akikaribia kufika hapo alishtuka akishikwa begani na kujikuta akihama njia upesi. Alipomwona aliyefanya hivyo, alijikuta akishusha pumzi na kumtazama.
                   "Haya  baba vipi siku hizi uandishi umebuma, au umetembea na  mke wa kigogo wakakufilisi hadi umekuwa kibarua  wa kiwandani", Mwanamke aliyemgusa alimwambia kwa dharau kuu., maneno  hayo yalikaribia kumfanya hata akaribie kucheka ila alijizuia na kuvaa sura isiyo na mzaha.
                     "Jamila shida yako  nini kwani? Ulisema unaachana na mimi ukinituhumu kwa umalaya wangu. Haya  kuniona nikiwa mfanykazi wa kiwanda wewe kinakuuma nini?"
                     "He! Heee! Unalo   babu weee, siyo wewe uliyekuwa ukijiona unavyowachukua kina dada kwenye kieskudo chako kile. Hivi sasa ndiyo umefikia  huku. Ama kweli kuna alfa na umega.", Binti ambaye si mfuatiliaji wa vyombo vya habari alijikuta akiongea hivyo, haswa baada ya kumwona akiingia mahala hapo akiwa namna hiyo ilihali anajulikana umaarufu wake. Akili yake ikawaza ni maarufu asiye na kitu kama wengine wenyee  kujulikana wana maisha ya duni, kumbe mwenzake yupo kwa ajili ya kingine.
                       "Haya ukimaliza uniambie niwahi kazini, niokoe kibarua changu", Kaila alisema
        
 
    Binti alimwaga maneno yenye shombo kwa Kaila,  alipoweka tu kituo wala  mzee wa kazi hakuhangaika kumsemesha. Alipiga hatua kuondoka huku akimwacha akiendelea kuangua kicheko, ambacho kwake aliona ni sawa na kumpigia honi kiziwi. 
     Msichana huyo aliwahi kuwa na uhuasiano naye, ila alikuja kuvurugana naye baada ya kumkuta na mwanamke mwingine. Alijaribu  kila aina ya uongo kuweza kumtuliza, ila haukuzaa matunda na hapo ndipo akajikuta akiwa na chuki kwake. Kumwona hapo kwa jinsi anavyopenda kumwona akiwa na hali mbaya, alikumbuka kumcheka na wala hakujua kama  bado jina lake lipo palepale. Atamaizi vipi juu ya hilo, wakati kutwa ni kwenye mitandao kuangalia umbea na wala si habari maalum. Ndiyo maana akakosa zote zinazomuhusu  hadi akafikia kumcheka hivyo, ilihali mwenzake anamwona ni punguani.
    Norbert alipompita alikaza mwendo na hatimaye akafika lilipo lango la  kiwanda, mahala hapo alikutana na mlinzi ambaye hakuonesha shaka naye. Alimpita tu na kuingia ndani, hatimaye akaja kufika kwenye eneo la ndani ambalo lina malori mengi yakiwa maegeshoni. Hapo aliishusha vizuri kofia yake kuzuia uso wake usionekane, aliingia ndani kwenye  moja ya idara za sehemu  hiyo.
     Kaila alitokea upande ambap hushughulikia haswa kutengeneza  viongozeo vya magari, huko ndiyo alidhamiria kuingia. Chipu  ile huwa na mahali huunganishwa, moja kwa moja aliposikia inatoka kiwanda hiko ndiyo akahisi moja  kwa moja  inaundwa idara hiyo. Kutokana  na watu wa humo asilimia kubwa kufanana mavazi hata wa idara tpfauti, aliweza kuingia bila wasiwasi
 
na akatokea upande ambao kuna   wafanykazi wakiwa kazini. Norbert aliwapita  wote  na akafika eneo ambalo kuna wengine  wenye kutumia  bisibisi   kufunga rimoti za magari. Napo aliwapita na kukuta mlango uliyooandikwa 'authorized only', huu aliuendea wala hakujali waliyomaanishwa kwenye maandishi yale ni kina nani.
     Aliusukuma mlango huo uliyoundwa kwa vioo, ukafunguaka akaingie eno lenye  korido yenye upana kiasi ikiwa na  milango ya kambarau kwenye kila pande. Norbert alipeleka macho kwa umakini kisha  akaishusha zaidi kofia kuhakikisha hakuna kiumbe anayeweza kuinasa   sura yake, alifanya hivyo kwa  kuhofia  kamera  za CCTV kuweza kuwepo eneo hilo. Alipiga hatua hadi alipofika mwisho wa korido  ile, huko alikuta ngazi zenye kushuka chini.  Bila ya kukawia alizishusha ambapo alikutana na mlango mwingine, huo uliandikwa  maandishi kama ya ule wa kwanza. Isipokuwa tu  kulikuwa na mlinzi mwenye kifaa cha  kuchunguza vitu vyenye asili ya chuma mwilini, akiwa na kirungu tu na  si kitu kingine.
                       "Hey! Sheria za hapa unazitambua wazi, huruhusiwei kufika huku  rudi kwenye idara yako", Mlinzi alimkoromea  huku akimsogelea, alipomfikia alimpelekea mkono kifuani akiwa na lengo la kumsukuma amrudishe alipotoka.
      Loh! Hakujua kama hilo ni kosa kubwa amelifanya, kitendo cha kumgusa tu Norbert. Kiganja chake kilidakwa kwa wepesi wa hali ya juu kisha Kaila akamvuta kuja upande wake. Mlinzi alijikuta akienda mzimamzima kama ajiletae kumkumbatia mzee wa kazi, alipokaribia kugusana kifua  na alimyefanyia kitendo hiko kwa wepesi  wa hali ya juu. Alijikuta akipitiliza baada ya Norbert kuyumba   pembeni, mlindaji aliapopita usawa  wa N001 alipokea pigo  moja la kisogoni akalegea  viungo vyote na kuanza  kuelekea chini.
      Norbert alimdaka kwa   haraka, aliangalia pande zote na kuona eneo hilo  halina kamera. Alimburuza hadi kwenye mlango mmojawapo wa  eleveta, hapo alibonyeza kitufe ambapo baada ya sekunde kadhaa ulifunguka. Alimsukuma humo ndani, kisha akaingia na kubonyez anamba ya ghorofa  ya mwisho ya jengo  lilipo juu yake. Alipofanikisha hilo alitoka upesi na kuiacha ifunge, Kaila akawa amemaliza   vikwazo vyote sasa akaingia kuelekea ndani.
      Mlango wa pili aliufungua akajikuta yupo kwenye chumba kidogo chenye mlango mwingine kwa mbele. Huku pembeni yake  kukiwa na kibanda chenye vioo, mzee wa  kazi alitupa macho pande zote na hatimaye akajitosa kwenye kibanda kilichopo pembezni ya hapo. Ndani alikuta kukiwa na tarakilishi ambayo inaonesha korido kadha ambazo hakuzipita, alpotazama pembeni alikuta mavazi ya mlinzi ambayo  aliyanyakua upesi.
Eneo kilipo kiwanda cha kufufua simu zilizokufa  Mbagala  charambe kwa Mbiku,  mahali ambapo kuna lango la kuingilia kiwandani hapo. Majira hayo bado gari za kampuni ya ulinzi ambayo ipo chini ya  umiliki wa Watson ziliingia mfululizo, vijana wenye silaha za moto walishuka kwa  wingi na kwenda kujipanga sehemu tofauti. Ujio huo wa watu hao uliwashangaza wafanyakazi wengi, ila hawakuwa na  uwezo wa kuhoji  waliendelea  na kazi zao kama kawaida.
     Muda mchache baadaye Huze aliwasili hapo akiwa na Watson, ulinzi imara waliyoukuta hapo baada ya kukagua waliona ungeweza  kutosha kummaliza  jasusi aliyewatia hasara kubwa  ndani ya siku mbili tu.  Hakuona kitu cha kuweza kuwafanya wamhofie tena, wao waliamini vijana hao wangemtia nguvuni. Hakujua  tayari wamechezewa mchezo mbovu, laiti kama wangelimaizi hilo wasingeliweka nguvu kubwa hapo na kuimarisha kule kwenye mradi wao mwingine.
                   "Vipi hapa Huze unafikiri huyo jasusi anaweza kutoka kweli kwa ulinzi huu?", Watson aliuliza.                    "Hawezi kutoka katu, vijana hawa shughuli yao naifahamu fika si ya mchezo", Huze alijibu, muda huo wapo sehemu ya juu wakiangalia jinsi ulinzi ulivyo mkali.
                    "Unajua hawa vijana serikali inajua ni walinzi wa kawaida  tu, ila ni hatari zaidi ya jeshi. Ukumbuke tumewapa mafunzo ya kijeshi na utumiaji silaha, huku wachache miongoni mwao wakiwa ni makomandoo"
                    "Ndiyo maana sina shaka nao, namsubiri huyo mshenzi mwenye kujifanya anajua kutumia silaha afike hapa. Ndiyo atajua kwanini tulipewa cheo na Alpha  cha kuweza   kuongoza kikosi hiki"
                    "Yaani hawa hata huyo N001 wanayeamini ni hatari, akiingia anga zao hawezi kutoka"
                    "Ok tuingie ndani kutazama  mfumo wa ulinzi ulivyo haswa kwenye kamera za  ulinzi", Huze alisema huku akigeuka nyuma  na kuelekea ulipo mlango wa kurejea ofisini.
 
**
 
 
    Eneo kilipo kiwanda cha kufufua simu zilizokufa  Mbagala  charambe kwa Mbiku,  mahali ambapo kuna lango la kuingilia kiwandani hapo. Majira hayo bado gari za kampuni ya ulinzi ambayo ipo chini ya  umiliki wa Watson ziliingia mfululizo, vijana wenye silaha za moto walishuka kwa  wingi na kwenda kujipanga sehemu tofauti. Ujio huo wa watu hao uliwashangaza wafanyakazi wengi, ila hawakuwa na  uwezo wa kuhoji  waliendelea  na kazi zao kama kawaida.
     Muda mchache baadaye Huze aliwasili hapo akiwa na Watson, ulinzi imara waliyoukuta hapo baada ya kukagua waliona ungeweza  kutosha kummaliza  jasusi aliyewatia hasara kubwa  ndani ya siku mbili tu.  Hakuona kitu cha kuweza kuwafanya wamhofie tena, wao waliamini vijana hao wangemtia nguvuni. Hakujua  tayari wamechezewa mchezo mbovu, laiti kama wangelimaizi hilo wasingeliweka nguvu kubwa hapo na kuimarisha kule kwenye mradi wao mwingine.
                   "Vipi hapa Huze unafikiri huyo jasusi anaweza kutoka kweli kwa ulinzi huu?", Watson aliuliza.
                   "Hawezi kutoka katu, vijana hawa shughuli yao naifahamu fika si ya mchezo", Huze alijibu, muda huo wapo sehemu ya juu wakiangalia jinsi ulinzi ulivyo mkali.
                    "Unajua hawa vijana serikali inajua ni walinzi wa kawaida  tu, ila ni hatari zaidi ya jeshi. Ukumbuke tumewapa mafunzo ya kijeshi na utumiaji silaha, huku wachache miongoni mwao wakiwa ni makomandoo"
                    "Ndiyo maana sina shaka nao, namsubiri huyo mshenzi mwenye kujifanya anajua kutumia silaha afike hapa. Ndiyo atajua kwanini tulipewa cheo na Alpha  cha kuweza   kuongoza kikosi hiki"
                    "Yaani hawa hata huyo N001 wanayeamini ni hatari, akiingia anga zao hawezi kutoka"
                    "Ok tuingie ndani kutazama  mfumo wa ulinzi ulivyo haswa kwenye kamera za  ulinzi", Huze alisema huku akigeuka nyuma  na kuelekea ulipo mlango wa kurejea ofisini.
 
**
 
                   "Bosi kuna faili hili muhimu inabidi lisainiwe upesi sana kabla hujandoka", Msichana mmoja alikuwa akitembea na kijana aliyevaa nguo nadhifu akiwa na mkoba mkononi. Binti huyu alishika faili pamoja na  kalamau akimwonesha.
                   "Aaah! Eliza mbona unalileta sasa hivi  nikiwa natoka kuwahi kikao cha bodi ya wakurugenzi. Muda wote ulikuwa wapi?"
                  "Bosi  ndiyo limewasili sasa hivi,  linahitajika kurejeshwa idara ya waajiri ni muhimu sana"
 
        Kijana huyo alichukua kalamu akiwa amesimama usawa wa mlango wa kamabrau, alisaini huku akimwambia   binti abonyeze kitufe cha kushuka cha lift hiyo. Alipofanya hivyo kengele maalum ililia, naye alimpatia  faili baada ya milango ya lifiti kufunguka.
                   "Jesus!", Kijana alijiseme kwa nguvu huku akiangusha mkoba wake kwenye mlango wa  kambarau, ndani alimshuhudia mlinzi akiwa   amelala chini hajitambui. Binti aliyepokea faili ndiyo kabisa lilimwanguka na akapiga kelele.
       Walinzi waliyopo eneo la karibu, walikuja haraka na kujionea hali halisi ilivyo. Kwa haraka  kengele ya hatari ilibonyezwa   huku  wachache wakikimbilia eneo ambalo wana silaha. Wengine walimtoa mwenzao kwenye lifti, wakiwa  mbele ya huyo bosi ambaye hakuelewa  kumetokea nini hadi akawa hivyo.
                    "Nasema hivi,  milango yote ifungwekwa kila idara. Walinzi wa  geti  kuu nao wafanye kazi yao.  Vijana nahitaji wenzenu wapekue humu ndani ya jengo zima,  hata idara nyingine   tujue kuna nini", Bosi alisema.
                     "Bosi!", Amri ilipokelewa na kwa haraka mlinzi aliongea kwa simu ya upepo, aliwapa taarifa wenzake waliyopo nje juu ya maagizo hayo huku wengine wakimpa huduma ya kwanza mwenzao yule hadi alipoamka.
      Mlinzi alizinduka  baada ya kuchomwa sindano kwa haraka aliponekana asingerejewa na fahamu muda ndani ya mfupi, alijikuta akitazama   hapo kwa sekunde kadhaa ndipo akajua yupo ghorofa ya juu mbali na ofisi  yake ya kazi, jambo  hilo lilimshngaza ambapo alichukua  dakika kadhaa ndipo alipoweza kukumbuka kile kilichotokea.
                       "Bosi tumevamiwa, kuna mtu amevaa ovaroli za  vibarua alifika na kunifanyia haya eneo langu la lindo", Alisema hata  bila ya kuulizwa,  maelezo yake yalifanya msako mkali uanze. Ikatolewa amri wafnayakazi wa idara ya rimoti za magari ya watoto wahojiwe juu ya hilo, wakifanya hayo hawakujua mtu wanayemtafuta yupo eneo gani.
 
ITAENDELEA



  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
Previous article
Next article

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4