Tuesday, 18 March

Ads Right Header

Buy template blogger

SEPTEMBER 1 SEHEMU YA SABA.


A Walk to Remember – Movie Recommendation | Bullies2Buddies
TULIPOISHIA SEHEMU ILIOPITA.

Mtoto akilia wembe   we mpe tu, sasa kapewa kweli na  umemkata. Yaani hata nafasi ya kujuta kwa kujiingiza kwenye mambo yaliyomzidi uweozo hatokuwa nao. Ndiyo kwisha habari yake, mpumbavu sana yule jamaa. Sasa tunamtoa sadaka halafu  tuone huyo mwenye kumlinda hadi kamwacha akalipukiwa na gari atafanya nini", Besi alijitapa baada ya kukamilisha kazi yake haramu.
ENDELEA NAYO SASA...

Mkuu  gari ya N001 imelipuka muda mfupi uliyopita,  hivi sasa ipo pale daraja la salenda ikiwa imegonga ukingo wa daraja", Afisa mmoja wa EASA alifikisha ujumbe harakaharaka kwa mkuu wake wa kazi, ambao haukufika kwa Katibu muhtasi kuhofia angeweza kumtia kihoro.
                      "Unasema! Tafuteni haraka alipo N001 naomba chipu yake itafutwe ilipo kama nayo imeharibika na mlipuko huo au bado ipo kwenye movement.
Nachohitaji ni kujua kijana wangu kama yupo salama  au lah!", CE alipopokea taarifa hiyo alibonyeza simu yake ya mezani wka haraka kisha akaongea, muda ambao bado aliyeileta hajaruhusiwa kuondoka.
                        "Mkuu bado ipo kwenye movement   sasa ivi inaonekana ipo Magomeni", Sauti kutoka kwenye  simu ya mezani ilisikika. Hii ilimfanya CE aachie tabsamu la ahueni kwa kujua N001 bado yupo kazini,  hakuwa amekumbwa na mlipuko ule. Alisema, "huyu anakuja ofisini hivi sasa nafikiri anahitaji huduma nyingine zaidi, kafika sehemu gani hivi  sasa?"
                      "Keshavuka magomeni hivi sasa yupo  Kigogo akielekea Ilala................Amefika Ilala hivi sasa  tujiandae ndani ya muda wowote anaweza kufika ofisini hapa....................................Yupo juu kwenye mlango wa kuingilia, ndiyo  anaingia ndani", Sauti ya mtu aliyepo chumba maalum  cha kufuatilia vifaa vilivyo miilini mwa wapelelezi, ilisikika ikitaja kila kituo alichofikia N001. Ilifanya hivyo kwa  dakika kadhaa  baada ya kuiona ikiwasili, CE alitulia kimya asikiliza hadi mdua ambao amesikia amefika  mlango wa kuingilia ndiyo akakata simu na kusimama wima.
                        "Wewe kazi yako  imeisha hivi sasa, rudi
kitengo chako N001 nitamsubiri mwenyewe hapo  kwa  hawara wake", CE alisema huku  akisimama, kijana aliyemletea taarifa naye aliinuka na wakatoka pamoja hadi walipofika  ofisini kwa Norene. Kaila walimwona ndiyo anaingia amechafuka  vilivyo, na miguu yake inanuka kutokana na kukanyaga maji machafu. Norene hali hiyo ilimshangaza mno, akaona mpenzi wake aliponea kwenye tundu la sindano huko atokapo.
                        "Naona mwenye masters leo umekutana na wenye PHD hadi wamekufanya hivyo, najua umeumia ila nahitaji maelezo ilikuwaje hadi gari lilipuliwe na bomu", CE alisema huku akifumbata mikono kifuani mwake.                          "Mkuu ukae utambue hapa nchini  kuna injinia hatari kuliko wote wa umeme, gari liliingiliwa system nzima ya   uratibu wake. Likawekwa bomu ambalo  lilihesabu  dakika kupitia kwenye  screen ya redio ya gari, nikapewa onyo ukisimama umekufa na ukipunguza mwendo hutopona. Ndiyo nikaamua kuchoropoka baada ya kujua kuna udhaifu mmoja,  haikuweza kuzuia mlango usifunguke hiyo system", Norbert alieleza huku akimtazama mpenzi wake kwa kuibia, aliuona uso wa binti huyo ulivyoingiwa na uoga.
                         "Hongera kwa kutumia akili vizuri, pia nikupongeze kwa kunibadilishia harufu ya ofisi na kuwa kama ya  sewage system. Norene mchukue mtu wangu akasafishwe huyo kama ana tatizo  atibiwe  huko, nahitaji akitoka hapa arejee kazini", CE aliongea   na alipomaliza alirejea ofisini akimwacha N001, Norene na yule kijana aliyekuja kutoa taarifa.
                        "Leo wamekuweza jamaa yangu, yaani ungechelewa   kidogo tu tungekuja kuokota minofu yako ikiwa imeivaa kama mishikaki", Kijana aliyekuja kutoa taarifa alisema huku akicheka kama vile kumetokea jambo la  kuchekesha, hata Norene naye alicheka kwani walishazoea kuwa namna hiyo mwenzao akipona kwenye tukio zito.
                        "We bwana kunuka  hebu kwanza twende huku,  hapa pua zangu zinakaribia kuharibika kabisa kwa hiyo harufu", Norene alisema huku akisimama..
                       "Na     leo          utageuka     bibi     kunuka nakwambia, yaani nakukumbatia hapahapa na mavumbi yangu haya na mijasho hii. Hadi harufu ya maji machafu ibaki mwilini", Norbet alisema huku akimkaribia Norene, akiwa ametanua mikono kabisa kujiandaa kumshika mwilini.
   Binti wala hakuonesha kumhofia alibaki akimtazma tu huku akicheka, alipokaribiwa kufikiwa kwa   wepesi wa hali ya juu. Alimpiga judo moja Norbert akaenda mzimamzima  chini, kijana waliyebaki naye mahala  hapo alicheka kwa nguvu mno huku akimtazama Kaila aliyenguka kifua.
 
      Norbert alijikuta akikumbwa na kicheko naye, pamoja na kuangushwa  kwa mtindo wa judo. Hakuona la kumfanya achukie ilihali alimfuata kizembe mwenyewe, huku akijua wazi wazi anayemwingia ni mwenye kuucheza mchezo kama yeye. Mambo yakuwa na mpenzi mwenye kufanya kazi  inayofanana, ndiyo hayo yamemtokea hadi akaangushwa chini. Alijiinua wima huku akiendelea kucheka, muda huo Norene alishaanza kupiga hatua kuelekea ulipo mlango wa kutokea ofisini humo.
      Naye alimfuata akiwa ameongozana na yule kijana, walitoka humo na kuingia kwenye eneo lenye ofisi nyingi kukiwa na wanausalama tofauti wakifanya  kazi zao. Kila mmoja aliyemwona Kaila na kuisikia harufu anayoitoa, alibana pua huku akicheka kwa nguvu kwani alijua wazi huko alipotoka alikutana na kioja cha mwaka. 
     Norbert aliongozwa na hadi kwenye vyumba vyenye mabafu maaluma ya kuogea, huko alioga kuondoa uchafu wote pamoja na harufu ya  mwilini. Alipomaliza  alipatiwa nguo ya ndnai tu, pamoja na taulo ambalo alilijifunga  kisha akaongozana na binti yule hadi kwenye chumba kingine chenye kufanana kila kitu na wodi ya hospitali. Humo ndani kulikuwa na kitanda katikati  sambamba na vifaa mbalimbali vikiwa vimepangwa kwa utaratibu maalum.
                   "Laza  mwili hapo, uniwekee mgongo juu", Norene alimwambia huku akivaa glovu za kitabibu.
                   "Ukinibaka je? Marinda yangu nayapenda" Kauali hiyo ilimfanya Norene  acheke, hata   mpira wa mkononi mmoja ukamponyoka na kuanguka.
                   "Mwone   kwanza, akili zako fupi  kama  kidole chako cha mwisho cha mguu", Norene alisema.
                    "Ndiyo  hizihizi umedata nazo hadi ukanipenda na kunizalia mtoto na miaka yote upo na mimi. Wacha ziwe fupi namna hii, zisiwe ndefu   wala  nyembamba sana kama ming'oko ya wamwera", Norbert alisema huku akijilaza kifudifudi kwenye kitanda, mikono aliweka  makalioni na kumfanya Norene acheke zaidi.
                    "Tahadhari kabla ya hatari, wewe tibu  hayo majeraha pembeni huko mgongoni. Ila huku wacha
nipazibe tu maana judo ile uliyonipa pale. Si bure una jinsia  mbili wewe", Norbert aliposema hayo, mlango wa mahala hapo ulifunguliwa kwa ghafla. Jambo hilo lilimfanya atoe mikono upesi makalioni, huku Norene akiwahi kuchukua dawa na pamba  baada ya kumaliza kuvaa glovu.
       CE alionekana akiingia   na alifunga   mlango, aliwatazama wapenzi hao wenye kuonesha wapo kwenye  kuhudumiana  kisha akaachia mgumo. Pamoja na hayo alisema, "N001 kuna chochote   ulichokiacha eneo la tukio ambacho kinaweza  kuwa alama ya shirika letu? Najua kwa jambo la haraka namna ile wewe ni binadamua pia, unaweza kusahau kitu ili kujiokoa"
                      "Pamoja na kuwa ni binadamua   bado akili yangu ilizinduka kutoka kwenye uoga. Nikaweza kuchukua kila cha umuhimu na kukiweka kwenye begi langu ambalo ni madhubuti",  Norbert alijibu.
                      "Safi sana,  umakini wa namna hiyo ndiyo ninautaka. Ukitoka hapa utapatiwa  gari  nyingine kama ile", CE alisema kumpongeza Norbert na aliuliza, "Waliyofanya   jambo hilo una uhakika hawakuacha alama yeyote ile ambayo ingeweza kukujulisha mahali walipo?"                        "Wameacha simcard na chipu ndogo  sana, vyote vipo ndani  ya begi langu. Nikitoka hapa  nitahitaji majibu yake. Muzo amevichukua kwa ajili ya kuvitafiti", Norbert alijibu na muda huohuo alijikuta akishtuka na kuuma maneno yake kisha akamtazama Norene aliyekuw aakiendelea kumtibu. Alimwambia, "we mwanamke utanishonaje  bila ya ganzi, ushaona ngozi ya robokopi hii. Nina neva za maumivu kama wengine"
        CE alijikuta akitabasamu na alisema, " ndo uanaume huo  uchomwe ganzi usubiri  iingie hadi uje ushonwe hapo begani ulipopasuka kidogo  itakuwa ni saa ngapi ukimalizwa  na unahitajika kurudi kwenye misheni. Kabla ya septemba tatu kazi iwe imeisha hii, okoa muda. Ngoja niwaache"
        Mkuu wa kazi alipotoka Norene alisema, "Nyoo yaani uweze kuvumilia maumivu ya kuchomwa kisu cha paja ulipojifanya umekufa kule Somalia ndiyo uje useme unaumia kwenye  kitu kidogo kama haki"
                         "Kwenye kujiokoa  na kifo unafikiri kuna nani anakumbuka kama anaumia, we sikia tu  siku ile  ningemwacha mwanangu yatima niliachiwa  kwa majaliwa  ya Mungu tu. Kuna mjinga mmoja alisema wanijaribu kwa risasi kama   nipo, mwingine ndiyo akakataa na kunichoma kisu kile kilichoniachia alama hadi leo. Ukikumbuka kifo maumivu unayasahau hata"
                         "Haya mimi nishamaliza kazi yangu, wewe nenda chumba cha mavazi ukajichagulie nguo  mimi naenda kuchukua funguo za gari utanikuta kwenye yard ya chini nakusubiri", Norene alisema huku akivua  mipira aliyoivaa.
                          "Kwanini tusiende wote ukanivalisha, tupige kwata kulekule kabla hujatoka"
                          "Nor hapana unaingia kazini wewe ukumbuke"
                          "Si nabusti mishipa ya fahamu kidogo, hujui  supu  bila  ya ndimu ni juisi ya moto  tu itakuwa"
 
**
 
       Habari ya kulipuka  kwa gari la Norbert  ilileta furaha kubwa mno kwa akina Huze. Wakabaki wakijiandaa   kwa lolote kuanzia muda huo, hawa kwenye maeneo ambayo kuna sehemu  zao maalum kwa ajili ya kuandaa kazi zao. Walijua lazima huyo mtu afike eneo ambalo kuna kituo  cha kutengenezea simu  za mikononi,  kwani kitu pekee walichohofia kingeweza kubaki kwenye mlipuko uole. Ni masalia  ya simutamba ile tu, si kingine.
                       "Sasa tumtarajie anaweza kufika kwa Mbiku kuanzia muda wowote ule huyo mpelelezi, simu ile haiwezi kulipuka yote. Pia ina alama ya kiwanda chetu cha kufufua simu zilizokufa", Huze alisema.
                       "Sasa huko ndiyo nimeshaagiza vijana wa  kazi wakae  mkao wa kula kwani  atafika muda wowote baada ya kujua hilo. Lazima tumnase huyu", Watson alisema.
                       "Jamani  naona tunafika  mbali sana, kabla ya kupanga mipango hiyo yote hebu  tufanyeni jambo moja. Tupate uhakika  wa kifo cha Kaila, tumelipua ndiyo na hata kwenye vyombo vya habari wametangaza  hilo. Ila haipaswi kujiamini namna hiyo", Besi alisema.
                       "Besi  kijana wangu mbona hii ishu imeisha tayari, unataka uthibitisho  gani mwingine. Hujui kama  ndani ya gari kumetolewa mwili mmoja, hata raia wameshuhudia  hilo. Unafikiri ndani ya gari lile kulikuwa na kiumbe gani kama si Kaila", Watson alisema.
                        "Kama ni hivyo  basi mchezo umekwisha, anzeni mpango haraka sana ninavyowajua wapelelezi hawalazi damu. Msije mkakaa hapa msubiri uchunguzi wajue simu  imetoka  kule, kumbe  keshaingia  na kusababisha mengine na akatoka. Hawa watu   wanafanya kazi  upesi  kama   kompyuta ya mamlaka ya  hali ya hewa. Wahi upesi sasa hivi, tena Huze ningependa uende kule kuifanya kazi hiyo  mwenyewe. Mimi narejea ofisini hivi sasa,  waziri wa nishati na  madini  pia ananihitaji  hivyo lazima niende huko"
                         "Ok hilo suala niachieni mimi", Huze alisema.
     
**
 
        Muda mchache baadaye Norbert alishavaa nguo nyingine, akiwa   ameshakabidhiwa gari mpya kwa ajili ya kuingia kazini kwa mara nyingine. Majibu juu ya chipu ile aliyoikuta ndani ya simu, yalitoka akawa na karatasi zenye kuonesha  kila kitu kuhusu kifaa kile. Alibaki mwenyewe kwenye yadi ya gari, akiwa yu ndani ya motokaa yake akipitia ripoti ile iliyotoka chumba maalum cha wataalamu wa tarakilishi.
         Maandishini aliweza kuona kifaa kile ni  mali ya kampuni yenye kutengeneza  magari ya kuchezea watoto ambayo hupatikana  Mikocheni. Huko  ndipo alipopanga kuanzia kwenye shughuli  yake baada ya kutoka hapo ofisini. Yaani ni tofauti kabisa na  kule ambapo kina Huze walidhani jasusi anayewatia hasara angefika, akili zao  ziliwaaminisha kuwa mlipuko ule  umeharibu chipu iliyopo ndani ya simu na vifa pekee vya simu ndiyo vitasalia.
       Hawakujua mwenzao ameruka tayari,  na ripoti ya kuonekana kwa mwili mule ndani haikuwa sahihi yote ni njama ya EASA kuweza kumuhadaa adui. Nao wameingia mkumbo uleule. Hakika walipumbazwa haswa kwa kuweka ulinzi kwenye kiwanda kingine, kumbe mzee wa kazi kalenga  pengine.
       Norbert alipomaliza kupitia ripoti nzima, aliiweka kwenye saraka ndani ya gari. Aliingiza namba maalum za siri za motokaa ile, kisha akaiwasha. Muda  lango maalum la kutokea humo lilishafunguliwa, alikanyaga akselereta kutoka humo ndani. Aliingia kwenye  njia ya chini ya ardhi  yenye kuzunguka kupanda kuelekea juu. Muda mfupi baadaye alitokea kwenye maegesho ya ghorofa la hoteli ambalo limebeba ofisi zao. Aliingiza gari  barabarani na kuondoka, huku akiwa amejua ni wapi pa kuanzia.
 
**
 
     Habari ya  kulipuka kwa  gari ambalo analitumia Norbert zilizagaa jijini, kwa mfululizo  wa matukio yaliyotokea kwa kipindi kifupi kilichopita. Wengi  waliona ni sehemu ya mwendelezo wa matukio ya kigaidi, hofu ilitanda na hata wengine wakagoma kupanda magari haswa ya jumuiya. Hata wale wenye kupenda kuegesha maeneo ya wazi walihofia kutegewa  bomu, hali hii ilipelekea kuibuke kwa  taaswira nyingine  nchini.
     Jambo  hilo likitokea mheshimiwa Waziri wa ulinzi, alikuwa kwenye kikao  kifupi na wakuu wa majeshi. Yaani mkuu  na manadhimu wake walikuwa kikaoni ofisini kwake, yote ni kuelekea siku muhimu maana siku zilibaki chache ndani ya mwezi agosti. Hivyo mambo yalihitaji kukamilika mapema. Dhima ya maandalizi  ilipangwa  na wanajeshi, huku mhandisi mzawa  akateuliwa kwa ajili ya kazi maalum maana mifumo yote  ndani ya chombo cha usafiri  katika uzinduzi kilihitaji umeme ili kifanye kazi.
                      "Mnajua muda  huu wa kupotea maafisa wetu na pia kutokea kwa amtukio mfululizo wa milipuko naanza kuona kunahusiana ", Waziri alisema.
                     "Hata mimi hilo nimeliona Mheshimiwa,  ila tuliache wenye kufa ya utafiti wapo kazini naamini watakamilisha kila kitu. Tujadili juu ya siku hii muhimu", Mkuu   wa majeshi  Jenerali Marwa alisema.
                       "Mheshimiwa waliyopewa kazi hii naamini hawawezi kutuangusha kwenye hili, Afrika ya mashariki hivi sasa tuna intelijensia imara mno. Nadhani ni muda wa sisi kuendelea na mengine. Maneno ya raia wanaona kama serikali inafanya uzembe wakati wangeachiwa  wao hii kazi wasingeiweza. Tuyaache yasituchanganye, sisi tuwe upande wetu na wengine wa kwao. Tusiingilie majukumu ya watu, kuhusika na usalama wa raia ni kazi ya polisi na kutafiti  mambo kama hayo kiintelijensi ni kazi ya EASA na TISS. Hebu nao watimize jukumu lao, tayari  taasisi mojawapo hapo ipo kazini", Luteni jenerali Belinda alisema.
                       "Ok, sasa jamani nadhani ni muda  wa kukagua vitu vyote kabla ya kuzinduliwa kwa safari hiyo. Tayari hivi sasa nimezungumza na Babu, wizara yake imeshampaa mtu wa kufanya kazi hiyo, reli imekaguliwa  bado kifaa chenyewe atakachopanda Mheshimiwa kifanyiwe hivyo. Maafisa wote  wa ngazi ya juu ndani ya jeshi, wawepo siku hiyo. Wote tutaenda na treni ya majaribio hadi Mwanza,  mabehewa yatawekwa ya kutosha.Ishu hii ilitakiwa kuwekwa watu wachache kwenye uzinduzi.Ila Mheshimiwa kapendekeza atembee na wananchi wake siku hiyo, tukae tukijua mabehewa yatafungwa mengi. Upande wa nyuma watawekwa wananchi wenye kusafiri kuelekea Mwanza tena  bure.
Hivyo kunahitajika behewa la mwisho wakae  vijana wenu.
Mbele     kwenye     kichwa     kutakuwepo     dereva     na
Mheshimiwa na maafisa wa TISS pamoja na nyinyi", Waziri alisema.
                       "Sawa Mheshimiwa kazi hiyo naiacha kwa Belinda chief of staff, ataamua kuongea na members of staff juu  ya hili", Jenerali Marwa alisema.
                       "Hakuna shaka ilimradi ulinzi  uwepo, jeshi la polisi watahusika katikati ya  mabehewa tu kwa kujichanganya na raia. Askari kanzu watawekwa humo, ili usalama wa raia uwepo. Safari hii nahitaji iwe ya kihistoria, iende na kumalizika kwa usalama mkubwa bila ya kukumbwa na lolote"
 
ITAENDELEA



  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4