Tuesday, 18 March

Ads Right Header

Buy template blogger

SEPTEMBER 1 SEHEMU YA TANO..



SEHEMU ILIOPITA...

Yaani kama ulivyosema atakuja, na kweli kaja kusikiliza na kuondoka mahala pale", Muki alijibu.                       "Vizuri sana vijana EASA  haikukosea haswa kuwapandikiza eneo lile muishi kama mateja. Nadhani umuhimu wenyewe ndiyo huu, kazi yenu imeishia hapa, mzigo wenu ushaingia kwenye akaunti zenu, ofisi imejua kama mmetumika kwenye misheni hii kwa ghafla"
                      "Tunashukuru  Bosi"

TUENDELEE NA

A Walk to Remember – Movie Recommendation | Bullies2Buddies
 **
 
       Watson na Huze walifanikiwa kufika zilipo ofisi za Kibolongo investment ambazo zipo  Posta jijini Dar es salaam. Baada ya kufanikiwa kuingia ndani, walimwita na Benjaamin ambaye alikuwa akiendelea na kazi  nyingine kama mwajiriwa   wa jengo hilo. Kikao  kifupi kiliwekwa, baada ya taarifa hiyo kufika   eneo hilo.
       Tukio zima ambapo kuna baadhi ya maeneo  Benjamin hakuhusishwa, aliweza kung'amua kila kitu kama kuna sehemu ya mpango hakuwekwa kwakuwa  yupo kwa ajili ya kazi nyingine tu na si kupanga namna ya kumteka mtu. Baada ya  kulisikiliza kwa umakini kuanzia siku iliyopita hadi kufikia asubuhi hiyo, ndipo akaona kuna kitu ambacho wenzake walikisahau na ni hatari mno.
                        "Unasema uliwapigia simu na kukuahidi kuwa wapo njiani?", Aliuliza kama ni mwenye kutoelewa.
                        "Ndiyo maana yake", Huze alijibu.
                         "ah! Ah! Ah! Huze umefanya kosa kubwa  sana bila ya kujielewa. Walimshika vipi na kuondoka naye, wakati uliposikia kule  ni kwamba walipojaribu kumvamia tu ndiyo wakaangamizwa na hao makirikiri. Hapa kuna  kachero wa TISS yupo kazini na ndiyo kacheza mchezo huu", Benjamin alisema.
                         "Besi umeongea jambo la muhimu mno, Huze hakuongea na mtu wetu bali ni mpelelzi huyu. Ni nani  sasa?", Watson alinena
                          "Hilo ni jukumu lako Watson kujua, ila
Besi  bado hunaniambia hatari hiyo ni ipi?", Huze aliongea.
                           "Kuongea naye maane yake maana yake namba yako kaiona, sasa jiulize kama kaforward call zote za kwako. Kama kadivert hiyo namba, basi ndiyo kasikiliza  simu zote ulizopiga siku iliyopita hadi kufkia hivi saa. Kama uliongea na watu wetu, basi tambua amejua kila kitu. Kufowadi simu siku hizi silazima uwe na simu ya mtu, utaalamu tu wa mitambo", Besi alifafanua.
                            "Cheki sasa hivi kama kuna mtu kadivert", Watson alimsihi.
                            "Namba za kuangalia sizijui mjue, yaani upande huo mimi ni mbovu haswa", Huze alisema.
                             "Piga *#62# kwa line zote mbili, kama
kuna kudivert sms au voice call kwa namba yako  uliyotumia kuwasiliana nao basi jua utaiona hadi namba iliyofanya hivyo",    Besi alimweleza Huze ambaye kwa haraka aliingiza hizo namba kwa haraka, sekunda chache tu aliweza kuona ripoti juu ya kuingiliwa mawasiliano yake na namba nyingine.
                              "Aaargh! Ku****e nipo diverted, huyu kunguru ni nani anayefanya hivi?", Huze alitukana na kisha akauliza juu aliyemfanyia hivyo.
                               "Huna muda wa kuhangaika kujiuliza hilo wakati bado line hiyo ipo kwenye simu yako. Vunja haraka hiyo line, ubadili namba na kila mtu kwenye mtandao afanye hivyo harka sana", Besi alishauri.
 
 
 
     Huze alifungua mfuniko wa nyuma wa simu kwa haraka, alichomoa kadi za simu kisha akaivunja papo hapo. Alishachachawa haswa akikumbuka idadi ya watu aliywasiliana nao tangu apewe taarifa   mbaya ambayo Kaila ameisambaza kwa afisa   wa jeshi. Loh! kama ni muda huo taarifa zake nyingi zishakamatwa, kiufupi alichelewa. ni mithili ya mtu aanzaye kuzima moto usiunguze suruali ilihali  sehemu ya kiunoni ya ngio hiyo ndiyo imesalia pekee.
                     "Huyu ni nani anayefanya  yote haya, inaonekana anajua nini atendalo", Huze alisema.
                      "That guy ni so brave inabidi ajulikane ni nani na tuwe naye kwa umakini zaidi. Hadi  kufikia hivi sasa jua keshajua taarifa zote za watu ambao umewasiliana  nao", Besi alisema.
                      "Iteni vijana kuanzia hivi sasa tuwe na ulinzi mkali, juu ya tu huyu tu", Watson alishauri.

Wakijadili hayo kumbe Kaila alishakamata  mawasiliano yoe ya Huze. Kibaya zaidi aliongea na wataalamu wa mtandao wakachapisha namba zote alizowasiliana nazo, zikiwa na majina   zilizosajiliwa kufanya kazi hiyo.  Aliona hiyo ndiyo sehemu pekee am,bayo angeweza kuianza kwa kuwatafuta hao mmoja baada ya mwingine, maana kila simu aliyosikiliza ilitoa taarifa na kuibuka kwa taarifa  juu ya  kupotea kwa maafisa wale. Hapo alijua lao moja, ingekuwa  ni jambo la maana kutowaacha na kuendelea kuwapekua zaidi. Watu aliyoambiwa ni wenye kuhusika, aliona ndiyo angeanza nao kwa siku hiyo haswa baada ya kufuatilia mawasiliano  yao na kujua ni wapi walipotoa taarifa juu yake.
    Baada ya kuachana  na kina Rambo, hatimaye alifika kwenye duka moja kubwa  la vito vya thamani lililopo maeneo ya Mwenge. Hapo aliingiza gari    hadi eneo la maegesho la ghorofa lililobeba sehemu hiyo yenye kuuza mapambo mbalimbali ya madini. Alishuka akiwa ni mwenye kujiamini, akaingia upande wa vyooni mwa jengo  hilo. Huko alihakikisha yupo pekee yake, ambapo kwa haraka alitazama   nje na kupo salama.
   Alitokeza nje ya dirisha na kusimama kwenye zege imara ya ghorofa   iliyopo uswa wa   bomba kubwa la kupitisha uchafu litokalo  vyoo vya juu. Norbert alijaribu kulishika  pitisho hilo la majitaka, alihakiki malighafi yake iliyotumika kuliunda na alipoona ni lenye asili ya chuma. Hakupoteza muda  zaidi, aliliparamia mithili  ya nyani, alilipanda  hadi alipofika ghorofa ya pili ya jengo ambapo kuna zege lililopo usawa  wa chini ya madirisha.
     Hapo  ndipo alipoishia na aliingia kwenye  fito ya zege, alitembea  nayo hadi alipofika eneo  lenye dirisha la choo ndipo akaingia ndani. Alijikuta yupo ndani  ya maliwato ndogo, ikionekana haswa ni kwa ajili ya ofisi moja. Mwonekano wake alibaini fika ni ofisi takamwili    kwa ajili ya mtu  mahsusi, haikuonekana hata kuwa ni  kwa ajili ya umma kamm kule alipoingilia.
     Alisimama hapo na kuingiza mkono   kiunoni mwake, alitoa bastola yenye rangi ya fedha ambayo aliifunga kiwambo cha kuzuia sauti. Aliiweka tayari kwa lolote kisha akafungua  mlango kwa  taratibu huku akichungulia  mahali alipotaka kuelekea. Norbert alitoka  baada ya kizingiti kufunguka nusu tu, alitokea kwenye korido yenye upana kiasi ambapo upande wa kulia  kwake kulikuwa na sinki la kunawia mikono ambalo juu yake kuna kioo. Kuwepo na ukuta upande huo ulimfanya aelekeze bastola wa haraka upande mwingine. Huko aliiona korido ikiwa na umbali wa mita moja tu, halafu ikikatika na kuonekana busati jekundu   halafu kwa mbele kidogo kukionekana  masofa yakiwa  yamepangwa kwa ustadi mkubwa.
     Nobert alipiga hatua za mnyato huku  kasiba ya sailensa yake  ikiwa mbele, alifika mwisho wa korido ambapo kwa  upande wa kulia kulikuwa meza yenye makabrasha  alianza kuiona  pembe yake. Hapo alizidisha mwendo kwa haraka, alipofikia akajitokeza kwa hara  na kuelekeza  bastola huko lakini  aliambua patupu na hakuona chochote.
    Mwenye ofisi   hayupo, akabaki pekee akiwa anashangaa samani za humo, Norbert alipokuta hali hiyo kwa haraka alianza kutembeza jicho  iwapo kuna kamera humo ndani ila hakuiona.
                 "Yuko wapi?", Alijiuliza lakini akiwa  amebaki na ulizo hilo,  alihisi sauti ya mtu akisogelea mlango, ambao upo upande yalipo makochi. Milio ya kukanyaga ardhi ilimfanya kwa  haraka  arejee  ajibane kwenye pembe moja ya ukuta, ambayo si rahisi kuonekana na mtu atokeaye upande  wenye makochi ambao ni sebule ndogo kuelekea ilipo  meza ya kazini.
     Mlango ulifunguliwa, na kufungwa kwa mara nyingine kisha ukasikia uruzi  pamoja na vishindo vya watu. Kaila alikaa tayari kwa lolote  lile, muda mchache baadaye aliingia mtu mwenye  suti ambaye alimpita na kufikia  kiti chake pasipo kutazama nyuma.  Alipogeuka aketi ndipo akakutana na   mzee wa kazi akiwa na chombo mkononi mwake, alijikuta akishtuka na kutaka hata kupiga kelele  ila aliwahiwa na kidole cha shahada kuwekewa mdomoni.
                  "Habari     yako     Mr     Pwaguzi,     nimekuja kukusalimia mara moja tu na rafiki huyu. Keti  kitini tafadhali",     Norbert     aliongea     huku     akitabasamu, alimwashiria mwenyeji wake aketi naye akatii. Aliendelea kusema, "nyanyua mkonga wa  simu hiyo umwambie sekretari wako hutohitaji mgeni kwa  hivi sasa"                    "Nitafanyaje hivyo wakati kuna mtu muhimu hapo nje ananisubiri nitoe  ruhusa aingie", Pwaguzi alisema  kwa hofu, kuelekezewa silaha ya moto haikuwa jambo la mchezo.
                    "Nimekwambia     fanya     hivyo,     unataka nikutandike moja  ya bega sasa hivi. Hii bastola hawatosikia  na kama kungekuwepo mtu aliyepo chooni naye asingeweza kusikia chochote. Epusha hatari kwako, fanya  hivyo. Sitorudia tena kukusihi kuhusu hili, ukichelewa sekunde kumi zijazo nitafumua  bega lako"
        Maneno ya Norbert yalimfanya kwa haraka ainue mkonga wa simu  na kubofya namba ya katibu muhtasi wake. Alitoa maagizo kama alivyohitajika kisha akatulia kitini akimtazama mgeni wake wa ghafla, hofu juu yake  bado ilikuwepo haswa majira hayo aliyosogea karibu kabisa naye na akaketi kitini mkabala.
                      "Pwaguzi, kwanini ulitahadharishwa juu yangu na Josi ambaye alipokea taarifa kutoka kwa Huze? Usalama wako ni kuongea tu ndiyo nitajua namna ya kukuokoa na mdomo huu wa bastola", Aliulizwa.
                       "Mpango  niliyopewa usije ukaharibika kwa ajili ya jambo hilo"
                       "Mpango gani na unahusika kwa namna gani na taarifa niliyoitoa?"
                        "Mpango wa kuhakikisha mheshimiwa anasaini mkataba mpya nasi juu ya mgodi wa almasi Kongwa. Wanajeshi wale wameshikiliwa kwa lengo la kumlegeza  nafsi yake, kwani nchi hii hakuna  vinara wa mabomu zaidi yao"
                        "Ili watege mabomu mapywa siyo   mkishikirikiana na Huze  bila uwepo wa Gera"
                        "Kaila unavyoona mimi maisha yangu yameelemea kwenye   almasi zile. Fikiria nitaishi vipi ikiwa Mheshimiwa  amegoma kuisaini  na amezuia  tani kumi za almasi huko bandarini kisa  kuna hujuma kwetu. Lazima tufanye hivyo mzigo wetu una thamani ya mabilioni ya dola"
                        "Vipi maisha ya hao mnaowatoa kwa hatia, yanalingana na  thamani ya huo mzigo? Uhai wa watu wasiyo na hatia kwa kutega mabomu maeneo ya mkusanyiko wa watu mnafikiri yanaweza kulingana na hicho mlikichuma kwenye ardhi yetu na mnakigombea. Si nyinyi mliyoanguka mahakamani mlipofungua kesi, sasa mmekuja na mbinu hii"
                         "Kaila hata wewe unaishi kwa ajili ya pesa na unafanya kazi yako ya uandishi kwa ajili ya pesa. Ina njia nyingi za kutafutwa na hii ni mojawapo, kila mtu na ngazi yake kwenye kusaka mafanikio"
                          "Ohoo! Pole sana kwa tamaa ya muda mfupi   ukiisaliti nchi yako ilihali ni mwenye kuheshimika kupitiliza", Norbert alisema huku akiishikilia bastola vizuri,
                          "No! No! No! Norbert hupaswi kufanya hivi, kumbuka mimi nina watoto watabakia na nani?"
                          "Mliyokuwa mkiwaua huko kwenye  mikusanyiko ya  watu, kwani hawana watoto. Iam sorry Pwaguzi, umeingia kwenye mikono ya N001 huwezi kutoka salama"
                         "Oooh No kumbe ni...." Pwaguzi alitaka kutoa kauli ila hakumalizia, alitobolewa paji lake la uso na risasi. Norbert hakutaka kumbakisha yeyote yule miongoni     mwa     wasaliti     wa     nchi,     alidhamiria kuwatokomeza wote. 
     Mahala hapo aliondoka upesi na kurejea kule maliwatoni, alitokea  upande wa dirishani na kushuka  na bomba lile lile hadi kwenye vyoo vya  umma. Huko aliingia kwenye  dirisha alilotokea na  kisha akajiweka sawa  na kutoka kwenye chumba cha choo ambacho aliufunga mlango muda aliyoingia. Alitoka kama vile hakuwa  mwenye kufanya tukio la kihalifu humo jengoni, alipitia kizingiti alichoingilia jengoni hapo na hatimaye akafika garini  ambapo alitokomea eneo hilo.
 
**
 
     Majira ya alasiri ofisi ya mwanasheria maarufu jijini, mwenye jengo hilo alisalia mwenyewe tu baada ya katibu muhtasi wake kuwa ameondoka. Alibakia akimalizia kazi ndogondogo ili naye aweze kutoka, hakuwa akijua hiyo siku haikufaa hata ifike. Aliona ni moja  mwendo wa wakati kuweza kutimiza majukumu yake ya hapa duniani, alipomaliza kila kitu akijiandaa kutoka nje  na mkoba wake.
    Mlango wa ofisi  yake ulifunguliwa, aliingia mzee wa makamo mwenye suti nyeupe huku akiwa  na mkoba mdogo mkononi mwake. Hakutarajia ujio wa  mtu huyo mahala hapo, kitendo cha kumwona alijikuta akijenga ndita usoni mwake kwani haikuwa  utaratibu kuweza kuwa na ugeni  majira hayo.
              "Mzee  tumefunga ofisi hivi sasa, njoo kesho tafadhali", Mwanasheri alisema huko akijiandaa kutoka humo ndani, kauli yake hiyo ilipelekea mzee huyo atumbukize mkono  kwenye mkoba wake kwa upesi. Aliibuka akiwa na  baastola  na kumwonesha, huku sailensa ikiwa imefungwa   barabara.
                "Wee ni nani?", Mwanasheria huyo aliuliza kwa uoga.
                "Mzimu wa mauti", Mzee  yule alijibu kisha akiuachia mkoba wake ukaanguka chini, mkono uliyokuwa umeushikilia ulianza kutoa kofia na kisha ukaondoa   ndevu nyingi nyeupe.
                 "Oooh! Shit Norbert Kaila"
                  "Unaweza ukaniita  N001 pia ukipenda, Mr Felix taaluma yako ya uwakili  haikuwa tatizo  wala hakuna sheria ya kukuzuia  juu ya kutetea wateja wako. Ndiyo maana ukaungana na mafisadi wa almasi kwenye mgodi wa Kongwa, walishindwa kesi yao  lakini ulionesha juhudi zako kama wakili. Watanzania wengi walikulaumu kwa kufanya kazi hiyo, ila ukweli utabaki palepale ni sehemu ya kazi yako na hata kulinda siri za mteja wako. Vipi kuhusika na mpango huu wa kulipua mabomu kwenye mkusanyiko wa watu nayo ni jukumu  lako, hadi ukapewa taarifa na Pwaguzi juu ya kuleta habari kwangu jeshini. Magari ya mwendokasi mawili yaliyobeba abiria wengi kupitiliza, miaka mitatu iliyopita mliyalipua yote"
                     "Kaila hapana kijana usiwe namna hiyo, naomba  tuliongee hili suala liishe. Seme nikupe  kiasi gani cha fedha, najua unahitaji kutafuta uwe na maisha bora kwa  ajili ya familia yako hapo baadaye. Tafadhali sana weka  silaha kando na uso tuongee""  Felix alisema huku akijaribu kupiga hatua kusogea mbele, aliyatamka akibabaika akiwa na lengo la kumshawishi Kaila maana kifo hakikuwa  na mwenyewe.
                     "Usidhani mimi ni mtu rahisi namna hiyo hadi ufikie kunihadaa kwa pesa, kama ni hiyo ninaipata nyingi kuliko  unavyofikiri. Moyo wangu haupo kwenye hela bali upo kwenye uzalendo. Rushwa ni adui wa haki, mtoaji na mpokea rushwa  vilevile ni adui wa haki. Lazima atokomezwe kwa gharama zozote, kwaheri Felix", Norbert alipomaliza maneno hayo, alimlamba risasi ya kichwa Mwanasheria huyo, ukawa ni mwisho wake wa kupenda kutafuta mafanikio kwa njia ya mkato.
       Alishamaliza watu wawili ndani ya masaa machache tu, aliondoka humo ofisini baada ya kujivalisha ndevu zile pamoja na kuiweka kofia kichwani mwake. Alipishana na mlinzi ambapo alimwaga akiongea kwa sauti ya kizee kabisa hadi  lilipo gari alilofika nalo, aliingia upande wa pili wa dereva kama vile ni mwenye kuendeshwa. Huko aliruka hadi kiti chenye usukani na kuliwasha  gari, uzee wa namna hiyo kumiliki gari ya kileo tena yenye baadhi ya alama ambazo hutumiwa na vijana. Kungeweza kumtia shaka mlinzi, na kujiuliza juu ya ujio wake mahala hapo. Ndiyo maana akaamua afanye hivyo kwa usalama wake,   tendo hilo halikuonekana  na mlinzi ambaye hakutilia maanani hata wakati anapifika hapo alilifanya.
      Norbert aliwasha motokaa yake, aliirudisha nyuma kisha akaielekeza upande lilipo geti. Aliliondoa mahala hapo  na  kuelekea  getini ambalo alipofika usawa wa mlinzi alilitoa kwa kasi isiyo kubwa kiasi cha kumfanya  asiwe makini kutazama kioo cha mbele kumuona akiwa yupo kwenye usukani. Vioo  vya pembezoni ambavyo ni vya giza, wala havikumpa shaka aliamini asingeweza kuna chochote. Aliingiza gari barabarani na kuondoka hapo akiwa ameacha maafa humo ndani, pasipo  kujulikana alisababisha kingine.   
       Walinzi walisubiri hadi ilipokaribia kuingia giza bosi wao hakuwa ametoka, jambo hilo lilifanya mmoja kwa haraka sana  aingie ndani kwenda kuangalia. Haikuwa kawaida kwa mkuu wao wa kazi kukaa ofosini hadi majira hayo ilihali hutakiwa kuondoka saa kumi na moja tu. Kijana  aliyefungua lango aliingia ndani kwa hima, eneo la katibu muhtasi hakukuwa na mtu yeyote hivyo alipitiliza moja kwa moja. Loh! Alimkuta Felix yupo sakafuni, sehemu ya kichwani ikionekana tobo alilopigwa risasi. Hali hii ilimchanganya lakini haikumtoa nje ya akili yake, kijana huyo pamoja na kupewa jukumu la kulinda ofisi hiyo hakuwahi kuona tukio la namna hiyo kwani siku zote huwa kazini na kumaliza  bila ya kushuhudia kioja. Alipagawa mno hata jasho lilimtoka kwa ghafla, ingawa alipatwa na nguvu ya  kusogea hadi ukutani na kubofya kitufe cha kengele ya hatari.
 
 
      Muda mchache baadaye walinzi kutoka kampuni ambayo inahusika kulinda jengo la  Felix, walifika kwa haraka na  kuweka ulinzi mkali kwa nje kama kuna mhalifu yupo ndani asiweze kutoroka. Wachache waliingia ndani na kuona kilichofanya kengele ya hatari yenye kuwaita kwa dharura kubonyezwa, loh! Tajiri mkubwa mwenye kulilipa shirika lao mamilioni ili wampatia ulinzi. Ndiyo huyo hahna uhai tena, wala aliyefanya hivyo hawamtambui.
       Mwenzao aliyepo zamu aliishia kuwaambia tu, juu ya aliyeingia hapo ndani kabla ya kuukuta huo mwili. Alieleza ni mzee  mwenye mkoba kuukuu, aliyekuja mara moja na kuondoka hapo. Hakuwahi  kumwona kabla, hadi aje kusema ni mwenye kumjua kiundani. Kibaya zaidi aliwaeleza hakuwa na miadi na  Felix, na muda aliyoingia ndani ulikuwa si wa kazi kwa mujibu wa ratiba ya ofisi hiyo. Alimruhusu kwa kuingia ndani baada ya kujitambulisha kama mjomba wa mwanasheria, amekuja mara moja tu kumwangalia. 
      Maelezo hayo hadi jeshi la polisi liliyachukua kwa muda huo, kisha wakawasiliana na ndugu wa karibu wa Felix kujua kama kuna mjomba wa namna hiyo, majibu waliyoyapata yaliwafanya waamini aliyeingia ni muuaji  hakuwa na undugu naye. Aliingia kutimiza jukumu lake tu na kutokomea eneo hilo, ikahitajika kuwepo mchoro  kwa mujibu wa maelezo ya mlinzi wa Felix.
 
**
 
                      "Jamani  inakuwa vipi watu wetu wawili wapoteze uai ndani ya siku moja tu. Huyu anayefanya haya ni nani?", Huze alisema akiwa amechachawa haswa, aliweka kikao akiwepo Watson na Besi ambao walipokea taarifa kwa pamoja juu ya tukio zima  lilivyo.
                       "Mnajua hii ni mbaya sana  yaani  kuelekea siku ya siku  tunachezewa mchezo na adui ambaye hatumjui", Watson alisema kisha akawatazama wote halafu akaendelea, "DG Gawaza amesema hakumtuma yeyote yule kwenye kazi  hiyo, hakuna mtu wa TISS aliyepo nyuma ya mchezo huo. Sasa huyu ni nani? Mkumbuke Professa Moses hawezi kunidanganya mimi, maana ni mshauri mkubwa   sana kwake kwenye masuala ya kiusalama na hata kuongoza taasisi ile". Mwanausalama huyu mstaafu alisimama kisha akanena, "Huze kuliko kuendelea kuendekeza hasira zako basi tambua tutakwama njiani kwenye mpango wetu na Alpha hatotuelewa. kabisa. Adui huyu lazima tumjue  ni nani ili tupate mbinu madhubuti ya kumdhibiti, mkumbuke kumtambua adui yako ni nusu ya ushindi"
                        "Mzee Watson umesema kweli, nashauri kufanyike jambo moja tu ili kumtia kiwewe  adui huyo mwenye kufanya haya. Naamini laini ya Huze ndiyo imesababisha yote haya, sasa basi tukubali kwanza anayehusika si TISS. Tumsake huyu kwa kumtia hasira naamini ataingia vitani akiwa  anajulikana, hivi mnaonaje kama tukimuua Norbert Kaila", Besi alishauri.
                          "Sasa  Kaila tukimuua bila   kumtia nguvuni  ndiyo itasaidia nini?", Watson aliuliza.
                          "Itasaidia haswa, naamini muuaji  wa watu wetu yupo kwenye ulinzi wake. Sasa sisi  tunafanya  tukio moja la kummaliza, halafu tunaacha alama ya kijinga ambayo naamini  itaweza kutusaidia kumpata huyo mtu. Hiyo alama itamfanya aje eneo  linalohusika nayo, sisi ndiyo tutamjua hapo na kutumia shambulizi la hatari", Besi alitoa rai.
                          "Wewe dogo unajua ni kichwa zaidi ya vichwa, nafikiri Cuba imezaa zao lile tulilokuwa tunalihitaji siku zote. Watson hukukosea kumpata mtu kama huyu aisee, kanifumbua macho. Huyu muuaji dawa ni hiyo tu hakuna namna nyingine, kumuua tu Kaila. Sasa basi  hivi, kesho kuna mkutano wa waandishi wa habari na waziri wa ulinzi Kaila ni mwandishi tena mwenye heshima kubwa, lazima awepo sehemu hiyo. Nataka kesho jua lisizame awe  marehemu, Besi  hiyo ni kazi yako", Huze alisema.
                           "Nitakachohitaji tu ni kujua nyendo zake hadi muda ambao atafika pale na si vinginevyo. Jukumu   lililobaki naomba mniachie mwenyewe, nafikiri   hivi sasa natakiwa niingie maabara nijue nitamwachia zawadi gani kwa ajili yake  hiyo kesho. Niwage", Besi alisema huku akiinuka kuondoka sebuleni hapo, alipeana mikono na wenzake na alitoka nje na kutokomea akiwaacha watu hao wameanza kupata ahueni  ya jambo linalowasumbua.
 
ITAENDELEA



  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4