BEFORE I DIE SEHEMU YA 4
“Kaka inocent kusema ukweli sijakwenda hospitali yoyote” Grace akasema kwa sauti ya chini
“Kwani siku ulipopima na ukakutwa umeathirika walikupa ushauri gani.Hawakukwambia kitu chochote? Innocent akadadisi
“Kusema ukweli kaka Innocent mimi sijakwenda hospitali yoyote kupima “
“Whaaat!!!….” Innocent akauliza kwa mshangao
“Unasema hujakwenda hospitali yoyote kupima ? Inno akauliza
“Ndiyo Kaka Innocent”
Jibu lile linamfanya Innocent avute pumzi ndefu.
“sasa umejuaje kama umeathirika ?
“baada ya kubakwa na yule mlinzi, kilipita kipindi cha kama mwaka mmoja na miezi mitatu hivi nikaanza kuumwa ,nikawa natapika na kuharisha.Nikaenda hospitali nikapewa dawa nikapona.Baada ya mwezi nikaanza kuumwa tena.Toka hapo homa za mara kwa mara zikawa hazikatiki,nikadhoofu na kukonda sana.Mama akaniambia tayari nilikuwa nimeshaathirika.Sikutaka hata kwenda hospitali kupima kwa sababu sikuona haja.Kama nilibakwa na mtu mwenye ukimwi basi ni wazi na mimi nitakuwa nina ukimwi
ENDELEA………………………………..
Innocent akakaa kimya ,akamtazama mbwa wake Pura akamshika shika kichwa na kumfanya Pura achezeshe mkia halafu akamgeukia Grace.
"My dear Grace,naomba unisikilize kwa makini.Kwanza naomba futa machozi”
Grace akafuta machozi yaliyokuwa yakimchuruzika halafu Innocent akasema.
“Grace,nina kila sababu ya kukemea uzembe uliofanyika ambao umechangiwa na mama kwa kuamini kuwa kwa vile ulibakwa na mtu mwenye ukimwi basi tayari na wewe umekwisha athirika.Sikutegemea kama mama ambaye ni mwanamke msomi na mwenye ufahamu mpana kuhusu virusi vya ukimwi na maambukizi yake aamue kutunga kitu ambacho hana uhakika nacho.Naomba nikufahamishe kuwa si kweli kwamba kila unapotembea na mwathirika wa virusi vya ukimwi basi na wewe tayari unakuwa mwathirika.Kuna sababu mbali mbali zinachochangia kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi kama utafanya mapenzi yasiyo salama na mtu aliyeathirika na virusi vya ukimwi, na kubwa zaidi ni iwapo kulikuwa na dalili zozote za mchubuko zilizosababisha damu ya mwathirika kupenya na kuingia mwilini mwako.Ninachokushauri kwa sasa ni kwenda hospitali kupima na kupata majibu yenye uhakika.Kwa sasa unaathirika kisaikolojia na kukufanya uendelee kuwa mgonjwa zaidi na mwenye kukata tamaa.Nakuomba dada yangu kesho uende hospitali ukapime na upate uhakika.Kama utakuwa umeathirika wapo wataalamu wa ushauri ,watakupa ushauri wenye kufaa ni jinsi gani unaweza ukaishi maisha yako ya kawaida ukiwa umeathirika.lakini yawezekana pia ukawa haujaathirika.Kama itakuwa hivyo tutaimba kwa furaha na kumtolea Mungu sadaka na utayaanza maisha mapya.Je uko tayari kwenda kupima na kuhakiki afya yako kesho?
Grace akakaa kimya kidogo akitafakari halafu akasema
“Nimekubali kaka Innocent.Nitakwenda kupima kesho na kuhakiki afya yangu.majibu yote yatakayotokea mimi nitayapokea kwa mikono miwili” akasema Grace.
“Nafurahi kusikia hivyo.Kesho baada ya kufika kazini nitamtuma dereva nitakayekuwa nimepewa aniendeshe ,aje akuchukue na kukupeleka hospitali yenye vipimo vya hali ya juu ili tupate uhakika wa afya yako.”
* * * *
Saa moja na nusu juu ya alama Innocent akawasili mahala pake pa kazi akiwa ameongozana na baba yake .Moja kwa moja bila kupoteza muda akapelekwa ofisini kwake na kukabidhiwa rasmi kampuni ile aiongoze.Mzee Ernest ngimanyu ambaye ndiye aliyekuwa akikaimu nafasi ya umeneja akakabidhiwa amwelekeze Innocent kwa undani juu ya utendaji kazi wa kiwandani pale halafu mzee Benard akaondoka na kwenda kuendelea na majukumu mengine.
“Mzee Ngimanyu ninaomba kabla ya yote niongee na wafanyakazi japo kwa dakika chache.Naomba uwakusanye wote tafadhali.” Innocent akaomba
Wafanyakazi walikuwa na hamu kubwa ya kumsikia meneja wao mpya atawaambia kitu gani,hivyo kazi zikasimama kwa muda na wote wakakukusanyika tayari kwa kumsikiliza Innocent.
“Tayari wamekusanyika na wanakubiri mzee” Akasema mzee Ernest
“Mzee Ernest unapenda sana utani.Mimi na wewe nani mzee? Innocent akasema na wote wakaangua kicheko kikubwa halafu wakatoka na kuelekea katika bwalo la chakula ambalo huwa linatumiwa pia kwa mikutano.
Mara tu alipoingia ukumbini akiwa ameongozana na mzee Ernest makofi yakaanza kupigwa na kumfanya Inno atabasamu kwa mapokezi yale mazuri.
Bila kupoteza muda mzee Ernest akasimama akaongea machache na kumkaribisha meneja mpya aongee na wafanyakazi.
“Ndugu wafanyakazi,nina furaha kubwa kusimama mbele yenu muda huu na kuzungumza nanyi.Kwa wale msionifahamu ninaitwa Innocent Benard na nitakuwa meneja wenu mpya kuanzia sasa” Innocent akakatishwa na makofi ya kushangilia yaliyopigwa na wafanyakazi.
“Nashukuru sana kwa makaribisho yenu mazuri ,nimejiskia faraja sana.Kwa kuwa nitakuwa nanyi kwa kipindi kirefu tutazidi kuongea na kufahamiana zaidi lakini kwa asubuhi hii ningeomba niseme machache.Kwa mujibu wa maelezo ya awali niliyoyapata toka kwa kaimu meneja mzee Ernest ni kwamba kwa siku za hivi karibuni kampuni yetu imekuwa haifanyi vizuri.Mauzo yamepungua na hivyo kupunguza kasi ya uzalishaji.Hii ni changamoto yangu ya kwanza kuishughulikia.Si changamoto ya kwangu tu bali ni yetu sote sisi kama wafanyakazi.Japokuwa kampuni hii inamilikiwa na mzee Benard lakini wadau wakubwa ni nyinyi wafanyakazi.Kwa umoja wenu mnaweza mkaipandisha kampuni au mkaishusha na kuiua kabisa.Ndugu wafanyakazi nataka tuanze upya ili kwa pamoja tuweze kupambana na hii changamoto kubwa ya kushuka kwa uzalishaji na mauzo.Nataka kila mmoja mahala pake pa kazi aone kwamba yeye ni sehemu ya kampuni na hivyo jukumu zima la uzalishaji ni la kwake.Nataka sote kwa pamoja tuwe na ari mpya ya kufanya kazi kwa bidii ,maarifa na ushirikiano.Ni silaha hii tu ya ushirikiano ndiyo itakayotuweka juu katika soko hili la ushindani mkubwa.Kwa kuwa kampuni hii ni yetu sote nawaahidi iwapo tutafanya kazi kwa bidii na kuogeza uzalishaji na mauzo,mishara yetu itapanda na kuboresha zaidi hali za maisha yetu kwani wote hapa tunafanya kazi kwa ajili ya kuwa na maisha mazuri ikiwa ni pamoja na kuwasomesha watoto wetu wapate elimu bora.Yote haya yanawezekana kama tutajituma katika kazi .Naamini yote yanawezekana kama kila mmoja atatimiza wajibu wake.Mwisho kwa kumalizia napenda kuwataarifu kwamba ofisi yangu iko wazi kwa mtu yeyote mwenye shida au matatizo mbali mbali.Nitapokea vile vile ushauri toka kwa kila mtu anayetaka kunipa ushauri ni jinsi gani tutaweza kuipeleka mbele kampuni yetu..Mwisho kabisa nawahakikishia kwamba pamoja kwamba kampuni yetu inapitia kipindi kigumu kwa sasa lakini hakuna mfanyakazi hata moja atakayepoteza ajira yake.Ahsanteni sana kwa kuniskiliza.”
Makofi,vigelegele vikalipuka ukumbini baada ya Innocent kumaliza kuongea machache.Kila mfanyakazi alikuwa amejawa na uso wa furaha na tabasamu kwa maneno yale machache yenye kujaa matumaini.Vicheko na kupongezana vikaendelea.Hii ikawa ni nuru mpya ya matumaini kwa wafanyakazi na kampuni .
* * * *
Akiwa ametingwa na kazi ofisini,mara simu yake ikaita.Alikuwa ni dereva wake Juma ambaye alikuwa amemtuma ampeleke Grace hospitali kwa ajili ya vipimo.
“hallo Juma nipe habari” akasema Innocent
“Bosi habari si nzuri.Nimemleta Grace hospitali ,amepata vipimo na baada ya kupewa majibu ya vipimo vyake ameanguka na kupoteza fahamu.Hivi sasa ameingizwa katika chumba cha huduma ya kwanza na madaktari wanamuhudumia”
Innocent akabaki ameishikilia simu asijue afanye nini huku kijasho chembamba kikimtoka.
“Juma nakuja hapo sasa hivi” Akasema Innocent kwa sauti yenye kujaa uoga ndani yake.Haraka haraka akainuka, akachukua gari la kampuni na kuondoka kuelekea hospitali.
“Yuko wapi Grace? Innocent akamuuliza Juma dereva aliyempeleka Grace hospitali
“Bosi ,Grace amepelekwa katika chumba cha huduma ya kwanza ,anapatiwa matibabu.” Juma akasema.Huku ameshika kiuno chake Innocent akauliza
“Hebu nieleze Juma nini kimetokea”
“Bosi kilichotokea ni kwamba nilimleta hapa Grace kwa ajili ya vipimo kama ulivyokuwa umeniagiza.Tulikuwa tumekaa wote pale wakati akisubiri majibu.Majibu yalipokuwa tayari akaitwa chumbani ili apewe.Ghafla nikaona mtu akitolewa na machela akikimbizwa katika chumba cha huduma ya dharura.Nikauliza nikaambiwa kwamba alipoteza fahamu baada ya kupewa majibu”
“Kwa hiyo hukuyaona majibu hayo” Innocent akauliza
“hapana Bosi majibu yake sijayaona.” Juma akajibu na kumfanya Innocent ainame na kutafakari kwa kina
“Kitu gani kitakuwa kimempelekea Grace aanguke na kuzirai? Yawezekana akawa amekutwa ana virusi vya ukimwi na kumfanya astuke ? Inawezakana kabisa akawa kweli ana virusi vya ukimwi.Masikini Grace namuonea huruma sana.Nitajitahidi kadiri niwezavyo kumpa faraja ili asikate tamaa”
Wakati akiwaza hayo madaktari wakatoka katika chumba cha huduma ya dharura wakiwa na nyuso za tabasamu.Haraka haraka Innocent akajitambulisha kama kaka wa Grace halafu Daktari akamwita ofisini kwake.
“Ndugu Innocent,kwanza napenda kukupa pole sana kwa mstuko uliokupata.natumai umestuka sana baada ya kupata taarifa za kilichotokea kuhusu dada yako”
“Daktari nilikuwa kazini na dereva wangu akanipigia simu kuwa dada yangu amepoteza fahamu ghafla.Ikanibidi kuacha kazi na kukimbia hapa mara moja.Hebu nifahamishe dokta ni kitu gani kilitokea? “ Innocent akauliza.
“Kwa ufupi ni kwamba Dada yako alifika hapa hospitalini kupima afya yake.Akaonana na daktari mhusika akaeleza anataka kupima kila kitu yaani kuanzia sukari,shinikizo la damu,virusi vya ukimwi n.k.Madaktari walimshughulikia na mara tu majibu ya vipimo yalipokuwa tayari daktari akamwita ili kumpatia majibu yake.Nafikiri ni ule uoga aliokuwa nao ndio uliopelekea yeye apoteze fahamu.Matatizo kama haya ni ya kawaida hasa kwa watu wanaokuwa na wasi wasi na afya zao hususan wanaokuwa na wasi wasi labda wameambukizwa virusi vya ukimwi.Tulimchukua tukampatia huduma ya kwanza na kwa sasa tayari amekwisha rejewa na fahamu zake ila tumempumzisha kwa muda na kama hali yake ikiendelea vizuri basi tutamruhusu arudi nyumbani.”
Innocent akatoa kitambaa na kujifuta jasho halafu akauliza.
“Daktari kwani majibu yake yanaonesha ana tatizo gani?
“Ndugu Innocent,siku zote majibu ya mtu huwa ni siri yake .Huwa haturuhusiwi sisi kusema matokeo ya majibu ya mgonjwa wetu kwa watu wengine.Nadhani ingekuwa vyema kama ungesubiri kwa ridhaa yake yeye mwenyewe akueleze.”
Innocent akamtazama daktari kwa sekunde kadhaa halafu akauliza.
“Dokta ninaweza kuruhusiwa kumuona?
“Bila wasi wasi.Unaruhusiwa kumuona.Ngoja nikupeleke”
Daktari akamchukua Inno na kumpeleka katika chumba alimokuwa amelazwa Grace.
“Grace kaka yako amekuja kukuangalia” Akasema daktari huku akitabasamu.
Grace alipomuona Innocent akapata nguvu ya ghafla akasimama na kumkumbatia kwa nguvu huku akilia.Innocent akazidi kushangaa.Daktari akafunga mlango na kutoka akawaacha Inno na Grace peke yao.
“kaka Innocent umekuja? Siamini kaka yangu.Walikwambia nimepoteza fahamu? Grace akasema huku akilia.
“Juma alinipigia simu na kuniambia kuwa ulipatwa na mstuko ukapoteza fahamu.Kulikuwa na tatizo gani?
Grace akakosa neno la kusema akakaa kitandani huku bado akilia.Innocent akakaa karibu yake akatoa kitambaa na kumfuta machozi.
“usilie Grace.hebu nieleze kuna tatizo gani?
“nashindwa hata niseme kitu gani kaka Innocent ” Grace akasema
“Kaza moyo.Nieleze.Niko hapa kukusaidia.Niambie tafadhali nini kimetokea? Majibu yanasemaje?
Grace akafungua mkoba wake na kutoa karatasi za majibu akampa Innocent.
“Soma mwenyewe,mimi sijui kiingereza.”
Innocent akaanza kuzipitia karatasi zile moja baada ya nyingine ghafla akajikuta akiachia tabasamu pana ,moyo ukaanza kumwenda mbio na machozi ya furaha yakimchuruzika.
“You are HIV negative…you are negative…ooh My God you are negative…” akasema Innocent
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………
LEGE
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 5
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Grace akakosa neno la kusema akakaa kitandani huku bado akilia.Innocent akakaa karibu yake akatoa kitambaa na kumfuta machozi.
“usilie Grace.hebu nieleze kuna tatizo gani?
“nashindwa hata niseme kitu gani kaka Innocent ” Grace akasema
“Kaza moyo.Nieleze.Niko hapa kukusaidia.Niambie tafadhali nini kimetokea? Majibu yanasemaje?
Grace akafungua mkoba wake na kutoa karatasi za majibu akampa Innocent.
“Soma mwenyewe,mimi sijui kiingereza.”
Innocent akaanza kuzipitia karatasi zile moja baada ya nyingine ghafla akajikuta akiachia tabasamu pana ,moyo ukaanza kumwenda mbio na machozi ya furaha yakimchuruzika.
“You are HIV negative…you are negative…ooh My God you are negative…” akasema Innocent
ENDELEA………………………………
Akamkumbatia Gace kwa nguvu huku naye machozi ya furaha yakimtoka.
“Grace huna ukimwi..huna ukimwi…Thank you God..thank you Jesus”
Innocent akasema kwa furaha huku amesimama na kumshukuru Mungu.
“Mungu baba wa mbinguni,ambaye kwako hakuna jambo lolote linaloshindikana,wewe unayeweza kutamka neno na kitu kikawa.Uliumba dunia na kila kilichomo ndani yake kwa kauli yako moja tu.Baba ninakushukuru sana kwa muujiza uliotuonyesha hapa leo.Umedhihirisha wewe ni mtukufu wewe ni mwenye enzi.Baba mwanao amekuwa akiteseka kwa muda mrefu akidhani ana maradhi haya ya ukimwi kumbe hana,baba ninashukuru kwa kutupa mwanga huu na kwa sasa baba wa majeshi ingia ndani yake na umfanye upya tena.Anapoenda kuyaanza maisha yake mapya baba mtume roho wako akae naye na kumuongoza katika njia zote njema na umbariki aweze kuwa na maisha mazuri yenye kukupendeza wewe peke yako bwana wa majeshi unayestahili kusifiwa na kuabudiwa,katika jina la Yesu ..Amen.
Baada ya maombi yale mafupi akatoa kitambaa akafuta machozi halafu akamwendea Grace aliyekuwa amekaa kitandani.
“Dada yangu ,bwana amekufungua na kukufanya mpya tena.Mwili wako ni safi na roho wake ataendelea kukuongoza.Hongera sana dada Grace.” Inno akasema huku akimpiga piga Grace mgongoni.
“kaka Innocent nadhani ni Mungu alikurudisha ili uweze kuyarejesha maisha yangu katika tumaini .Nimeteseka vya kutosha na nilikwisha kata tamaa ya kuendelea kuishi tena.Sijui hata nitakulipa kitu gani kaka Innocent kwa sababu wewe ndiye mtu wa kwanza kunipa ushauri wa kuja kuangalia afya yangu…” Grace akaendelea kulia.
“Nyamaza kulia Grace.hutakiwi kulia tena.Unatakiwa uyaanze maisha mapya ya furaha na amani.Leo umekuwa kiumbe mpya.”
Innocent akaenda kuonana na daktari na kumuuliza kama anaweza akaruhusiwa kuondoka na dada yake.Daktari akamruhusu,wakaingia garini na kuondoka.Wakiwa ndani ya gari Innocent akapiga simu nyumbani kwao iliyopokelewa na Sabrina.
“Hallo Sabrina nataka leo jioni uandae chakula safi.Chinja kuku andaa chakula kitamu kuna jambo kubwa na zuri la kusherehekea jioni ya leo kama famila.”
Mchana huo Innocent akawa akizunguka katika maduka mbali mbali yanayouza nguo na urembo,akawanunulia Grace na Sabrina nguo pamoja na kumpeleka Grace saluni ambako alipambwa ,akapambika,kiasi kwamba kama ulimuona asubuhi basi ungempotea katika muonekano huu mpya.
“wow ! I knew it you are so pretty.I knew it” Innocent akaongea kwa mshangao mara tu baada ya kumuona katika muonekano mpya.Grace hakusema kitu akabaki akitabasamu.
“Umependeza sana Grace.”
“ahsante kaka Innocent. “
saa kumi na mbili za jioni wakawasili nyumbani.Innocent akamfungulia mlango Grace akashuka.wa kwanza kumuona alikuwa ni Sabrina,akastuka sana.
“ouh Grace ni wewe kweli? Umebadilika ,umependeza sana.Sukujua kama ni wewe.”
Kabla Grace hajajibu kitu mama yake Innocent akatokea akiwa amefura kwa hasira.
“Na wewe umekuwa bosi siku hizi mpaka unarudi saa hizi? Unategemea kazi za nyumbani akufanyie nani? ….
“Mama nilikuwa nimekwe……….”
Kabla Grace hajamaliza kujibu Innocent akadakia.
“Alikuwa na mimi mama.Nilimpeleka hospitali na baadae nikampitishia saluni.Grace nendeni ndani”
mama yake akamwangalia Inno kwa hasira akasema
“Nakwambia unachokitafuta kwa huyo Malaya utakipata.Kila siku ninakuonya usiwe karibu na huyo chokoraa hutaki kusikia”
maneno yale yanamuudhi Innocent akajibu.
“mama tafadhali usimuite Grace Malaya.Huyu ni sawa na mwanao.Amekukosea kitu gani mama? Au anavyokaa hapa anakunyima kitu gani?
“Usinijibu hivyo Innocent.Naona huko Ulaya ulikotoka wamekufundisha vibaya sana.Wewe si wa kusimama na kuanza kujibizana na mimi.” Mama yake Inno akasema kwa hasira
“Sijibizani nawe mama yangu,ila ninajaribu kukuelewesha kuwa hawa Grace na Sabrina ni sehemu ya familia yetu…. Kabla hajamaliza kaka yake Edson anatokea.
“Wow brother” akasema Inno kisha wakakumbatiana kwa furaha.
“naona mzungu umerudi nyumbani” Edson akatania wote wakacheka.
“Vipi mbona nasikia makelele huku nje? Edson akauliza
“Huyu mdogo wako toka amekuja amekuwa akiwapa kiburi sana hawa wasichana.Toka Inno amerudi wasichana hawa wamekuwa na kiburi hawataki kunisikia hata kidogo.Muonye mdogo wako akae mbali na hawa wasichana” mama yake Inno akasema kwa ukali
“Inno mbona unamkorofisha mama namna hiyo? Edson akauliza
“Si hivyo brother ,tatizo ni kwamba hawa wasichana wanakaa humu,wanasaidia kazi za ndani lakini hakuna mtu yeyote anayewajali.Wamekuwa wakinyanyaswa na kubaguliwa kitu ambacho mimi, sikipendi”
Edson na Innocent wakaingia ndani na kumuacha mama yao pale nje amefura kwa hasira.
Saa mbili za usiku tayari meza ilikwisha andaliwa.Kila mmoja alikuwa akijiuliza nini ilikuwa sababu ya furaha ile ya Innocent. Innocent akaleta shampeni akaweka mezani halafu familia yote ikakusanyika mezani kwa ajili ya chakula cha usiku isipokuwa Grace na Sabrina ambao wao hulia chakula chao jikoni.kabla hawajaanza kula Innocent akasema
“jamani kabla hatujaanza kula chakula hiki,napenda niwafahamishe kwamba chakula hiki ni mahsusi kwa ajili ya kusherehekea mwanzo wa siku mpya na maisha mapya ya mmoja wa wanafamilia hii.”
Kila mmoja akamkazia macho Inno bila kuelewa alikuwa akimaanisha kitu gani.
Innocent akaenda jikoni na kuwaleta Grace na Sabrina akawakaribisha mezani.
“baba na mama,kaka Eddy na dada sarah,leo mmoja kati ya dada zetu hawa ameyaanza maisha mapya .Grace leo amepima afya na amekutwa hana maambukizi ya virusi vya ukimwi.Yuko mzima kabisa na ushahidi huu hapa”
Innocent akasema na kuweka mezani karatasi za majibu ya vipimo toka hospitali .Kila mmoja akapigwa na butwaa.
“Napenda tokea sasa mtambue kwamba Grace si muathirika wa virusi vya ukimwi na kwa maana hiyo basi anaanza maisha mapya na ningeomba watu wote humu ndani tumpe ushirikiano katika maisha mapya atakayoyaanza.Ni mapema bado kusema ni maisha ya namna gani atayaanza kwa sababu bado naangalia ni kitu gani cha kumsaidia ili aweze kuyaendesha maisha yake.”
Innocent akafungua shampeni wakashangilia na kumpongeza Grace isipokuwa mama yake Inno aliyekuwa amefura kwa hasira.
* * * *
Siku nne zimepita toka Grace alipopima afya yake na kujikuta hana maambukizi ya virusi vya ukimwi.Maisha yake yaliendelea kuwa ya furaha japokuwa bado alikuwa akikumbana na vikwazo vingi toka kwa mama yake Innocent.Kwa kufuata ushauri wa Innocent aliendelea kuwa mtulivu na mvumilivu wa manyanyaso yote aliyofanyiwa.
Ni siku ya alhamisi asubuhi na mapema,Innocent akijiandaa kupanda gari tayari kwa kuwahi ofisini,Grace akamfuata mbio.
“Kaka Innocent samahani kwa kukusumbua.Unajua toka umeanza kazi umekuwa haupatikani sana hapa nyumbani.Wiki yote hii nimekuwa nikitafuta nafasi ya kukuona na kukwambia kuwa nina maongezi na wewe pindi upatapo nafasi.Naomba kaka Innocent ukipata nafasi hata muda wa jioni uniambie nina maongezi na wewe ya muhimu” Grace akasema huku akitazama chini.Innocent akamshika bega na kumwambia.
“Usijali Grace.Kwa sasa nina kazi nyingi sana ofisini lakini nitajitahidi kutafuta muda ili tukae tuongee.Vipi lakini maisha yanakwendaje hapa nyumbani?
Huku akijitahidi kuuficha uso wake Grace akajibu
“Hapa nyumbani maisha ni kama kawaida.Nimeshayazoea”
“Sawa , Grace ngoja mimi niwahi ofisini halafu nikipata muda tutakaa tutaongea.”
“Ahsante kaka Innocent.Kazi njema”
Innocent akaingia katika gari lake na kuondoka kuelekea kazini.
“Nimeanza kuyaona mabadiliko kwa Grace.Kwa siku hizi chache toka apate majibu ya vipimo vyake amebadilika sana.Ninaiona nuru ya matumaini katika macho yake.Ninaona ni jinsi gani alivyo na shauku ya kuyaanza maisha yake mapya niliyomuahidi.Ni lazima nimsaidie binti yule ili aweze kutimiza ndoto zake maishani.” Innocent akawaza akiwa ndani ya gari kuelekea kazini.
Kwa siku chache toka Innocent alipokamata uongozi katika kampuni hii ya kutengeneza maji ya kunywa,hali ya kiutendaji imebadilika sana.Wafanyakazi wamekuwa na mwamko mkubwa wa kufanya kazi kwa bidii wakiwa na matumaini makubwa ya kuboreshewa mishahara yao ahadi waliyopewa na na kiongozi wao mpya.Mabadiliko haya ya utendaji kazi miongoni mwa wafanyakazi yalimpa moyo sana Innocent na kumfanya aamini kuwa muda si mrefu uzalishaji utaongezeka na hivyo kuboresha zaidi hali za maisha ya wafanyakazi.
Asubuhi hii wafanyakazi wote walikwisha wahi katika sehemu zao za kazi na kazi iliendelea kufanyika.Innocent akasalimiana na baadhi ya wafanyakazi halafu akaingia ofisini kwake akaendelea na kazi zake.Akiwa ofisini kwake mara kwa mbali akasikia kama kuna mabishano katika ofisi ya katibu muhtasi wake,akaacha alichokuwa akikifanya akafungua mlango na kumkuta katibu wake akibishana na mama mtu mzima ambaye ni mmoja kati ya wafanyakazi wa kampuni hiyo.
“Kuna nini hapa Devotha? Innocent akauliza.
“Bosi kuna huyu mama hapa amekuja analazimisha kutaka kukuona nikamuuliza kama ana miadi na wewe akasema hana nikamuuliza ana shida gani akasema ni shida binafsi,basi ndiyo nikawa najaribu kumuelewesha utaratibu ulivyo wa kukuona lakini yeye bado hanielewi.” Devotha katibu muhtasi wa Innocent akasema.
“Basi mruhusu mama aingie ofisini.halafu Devotha usimzuie mfanyakazi yeyote kuja kuonana na mimi.Awe na shida yoyote ya kiofisi au binafsi.Kama nipo mruhusu kila mtu anione.Sawa?
“Sawa bosi” Devotha akasema huku akionyesha kuchukizwa na kitendo cha mama yule kubishana naye hadi akakutwa na bosi wake.
“Mama shikamoo.” Akasema Innocent huku akimuelekeza mama yule aketi kitini.
“Marahaba baba.habari za kazi”
“Habari za kazi nzuri mama yangu..Karibu sana sijui una tatizo gani?
“Baba mimi naitwa Mama Sophia.Ni mfanyakazi wa kampuni hii,sisi ndio tunaosafisha chupa za kuwekea maji.Mimi ni mjane na nina watoto wanne.Tatizo nililonalo baba yangu ni kwamba mwanangu wa kwanza ameshindwa kwenda shule kutokana na ukosefu wa fedha.Amechaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano katika shule ya bweni lakini mpaka sasa hivi ninavyokueleza ni kwamba hajafanikiwa kwenda shule kutokana na kukosekana kwa fedha ya kulipia huko shuleni.Nimekuja hapa kwako baba uone ni jinsi gani unaweza ukanisaidia ili mwanangu aweze kwenda shule kuendelea na masomo.Ikiwezekana naomba nikopeshwe fedha halafu nikatwe katika mshahara wa mwisho wa mwezi.Naomba unisaidie baba kwa sababu hapa nilipo niko mwenyewe sina msaada toka sehemu yoyote ile.Kazi hii niifanyayo hapa ndiyo kila kitu kwangu.”
Mama Sophia akajieleza kwa upole.Innocent akamsikiliza mama yule kwa makini na aliyoyasema yakamuingia moyoni,akamuonea huruma sana mama yule mjane.
“mama nimekusikia.Kwanza pole sana kwa matatizo na vile vile nikupe hongera kwa kuweza kumudu kulea na kuwasomesha watoto wako wote wanne wewe mwenyewe.Nakupongeza kwa sababu elimu ndiyo msingi bora wa maisha yao.Mama kwa kweli suala lako limenigusa sana.lakini pamoja na kuguswa huko mama yangu napenda nikufahamishe kuwa kwa sasa hali ya kampuni si nzuri kifedha kama nilivyowaeleza siku chache zilizopita.Nina imani kuwa kwa siku chache zijazo uzalishaji ukiongezeka basi tutakuwa sehemu nzuri kifedha.Pamoja na hayo mama yangu hebu niachie suala hili ili nione ni jinsi gani ninaweza kukusaidia.Naomba unipe siku ya leo nishughulike na suala lako.Hata kama nikikosa nitajitahidi kutafuta sehemu yoyote ile ili tufanikishe mwanao aende shule.Mama fedha hizo zitakuwa si mkopo bali nitakusaidia kama mama yangu .”Innocent akasema
“baba nashukuru sana kwa msaada wako.Sijui hata nikushukuruje lakini nakuombea kwa Mungu akubariki na kukuzidishia kwa moyo wako wa huruma.” Akasema mama Sophia huku akisimama na kuondoka.
“Kuna kila sababu ya kuboresha maisha ya wafanyakazi.Huyu mama amekuwa jasiri kuja kunieleza tatizo lake,lakini nina imani kuwa wapo wengine ambao hawana ujasiri wa kunieleza matatizo yao.Nitajitahidi kwa kila niwezavyo kuboresha mishahara na stahili zao nyingine ili maisha yao yaweze kuboreka.” Innocent akawaza. Halafu akaendelea na kazi .
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
Previous article
Next article
Leave Comments
Post a Comment