Wednesday, 19 March

Ads Right Header

Buy template blogger

SEPTEMBER 1 SEHEMU YA KUMI NA TATU.


Why Do Black Women Experience More Pregnancy Loss?
TULIPOISHIA..

Norbert alifika hadi kwenye soko  la mitumba la Karume, hapo alinunua  kofia nyingine kisha akaondoka kurejea katikati ya jiji mahali ambapo aliliegesha  gari lake kabla hajaamua kumvamia Huze. Mpango wake wa kumteka nyara  tajiri yule, ulishindikana hapo kwa jinsi alivyovamiwa na walinzi.

ENDELEA NAYO ...

**
 
      Baadaye Huze alirejewa na fahamu alijikuta akiwa yupo  kwneye   wodi ambayo ina ulinzi mkali, akili yake iliporejea sawasawa ndipo maafisa wa jeshi la polisi walifika mahali hapo na kumuhoji juu ya tukio lile lililomkuta. Kutokana na jinsi  ilivyokuwa ilimbidi atumie uongo mwingi  kwa  kuunda kisa chenyewe hadi anafanikiwa kupoteza fahamu. Walinzi nao waliungana naye kwenye maelezo, walieleza kinamna ambayo walishabihiana na bosi wao  na  hakuna kitu kilienda kinyume.  Askari wakaamini Huze alivamiwa  na mhalifu ambaye hamfahamu, wakajaza maelezo  hayo kuanza upelelezi wao. Ukosefu wa kamera za usalama  barabarani, uliwafanya wasigundue  kilichokuwepo pale, pia namna ambavyo tukio lilivyo hakuna raia wa kawaida  aliyethubutu kutia  macho yake  na  baadaye aje kuwaeleza maafisa  hali halisi.
      Majira ya jioni ya siku  hiyo, aliruhusiwa na alirejea nyumbani kwake ambapo ulinzi uliimarishwa  na walinzi wa kampuni yake baada ya kukataa kuchukua maafisa wa TPF akisema walindaji wao wanaweza kumwokoa. Watson alikuja kumwona   akiwa na Kanali pamoja na Brigadia wenye kuhusika nao kwenye usaliti wa nchi.
                "Unajua  sisi tumesikia maelezo ya  upande wa jeshi la polisi tu, ila hatukufanikiwa kujua kuhusu huyo mshenzi, hata walinzi hawakumwona. Uliyemwona ni wewe tu ambaye umepoteza fahamu pekee, sasa tunataka kusikia kutoka kwako Huze. Ni nani huyo mwenye kufanya hayo",  Watson alisema.
                 "Jamani! Jamani mjue kuna mjusi mmoja hatari sana yupo  nyuma yetu na keshanusa kila kitu", Huze alisema.
                 "Mafumbo si mahali pake Huze, weka kila kitu wazi", Brigadia alisema.
                 "Ok ni hivi, ushenzi wote huo kaufanya Norbert Kaila. He still alive hakufa na bomu lile, sasa jamani tujue huyu mtu  ni nani? Kwa  nilivyosikia alivyotoroka  tayari ni komandoo, yupo nyuma ya nani jamani. Brigadia na mwenzio Kanali, upande wa MI  mnaujua vilivyo, Watson upande wa TISS unaufahamu, kuna rekodi  za huyu mtu kwneye ufanyaji kazi?"
                  "Norbert Kaila si mwanajeshi wa JWTZ na hakuna special force mwenye jina kama lake. Tukianza  kazi hii, nilipitia rekodi ya kila special force wa MI ila  sikuwahi kuona jina  hilo", Brigadia alisema
                   "Anayoyasema Brigadia ni kweli kabisa, rekodi yake ipo tu  kwa kuwahi kupitia mafunzo ya kijeshi ya JKT na alitakiwa kuajiriwa kama angeenda Monduli ila mzazi wake marehemu Brigadia Alphonce Kaila   alipinga hilo ndipo akaenda kusomea uandishi huyu. Kuwahi kupitia kwake mafunzo tunajua wachache tu, hakuna mwingine anayefahamu miongoni mwa raia", Kanali alisema.
                  "Pia kiupande wangu rekodi zote za TISS nazifahamu fika, Norbert Kaila si mtu wa kwenye system labda awe informer wa mtu  aliyepo  kwenye system na si vinginevyo", Watson alisema.
                   "Sasa huyu mtu yupo upande wa  nani? Au EASA hawa, na wameingia vipi kazini hawa washenzi. Mkumbuke hawa ndiyo chanzo cha kukamatwa kwa kaka yangu, inabidi tuwe nao makini zaidi"
                    "Hilo la muhimu zaidi, mimi natoka hapa na kwenda     nyumbani     kwa     DG     wa     TISS     naenda kumchokonoa zaidi maana tulipanga niende kuchukua kitambulisho kesho cha kusafiri  na treni. Ninaweza kupata kitu, maana  Moses na Kaila ni marafiki", Watson alisema.
                     "Watson unaelewa plan yetu ilivyo   umekubali vipi kuchukua tiketi ya lile kopo lao. Are you out of your mind?"
                      "Huze cool down, wewe hakikisha  helikopta zetu za kutoroka nchi hii ipo ok. Njia ya kuondokea ni    mashariki kwa  bahari ya Hindi tu, meli   ya Alpha ipo jirani na visiwa  vya komoro. Hapo ndiyo tutaenda kuweka kituo chetu cha safari, Gera naye  ataondoka na rubani tu, akifika angani anamuua kisha anakamata chombo kuufata  mwenyewe", Watson alisema.
                       "Nilitaka nishangae ujue, yaani Watson huyuhuyu  akubali kupanda kopo lile,  jamani kwanza hapa tugawane majukumu. Alpha anaingia leo hii   saa tatu usiku huu, naomba Brigadia   ukamchukue na kumpeleka mahali stahiki. Watson unaweza kuendelea na  mpango wako wa kumchimba DG. Tena wakikubali masharti yetu nafikiri mnaju nini cha kufanya"
                       "Kazi ya bomu ni kulipua, hakuna ambaye atashughulika  kulizima. Bomu kalitengeneza Besi password ukaweka wewe, kuactivate unafanya wewe. Unafikiri nani ataweza kulitegua, bomb  squad wote wauawe kwa bomu tukimaliza kila kitu chetu Besi keshaseti  mambo kule na mteguaji ni yeye tu hakuna mwingine mwenye kuliweza hilo", Kanali alisema
                       "Tuanzeni majukumu mara moja  jamani, mimi napumzika hadi saa sita usiku kisha nitakuja kuonana na Alpha", Huze alihitimisha  kikao  hicho, baada ya kukubaliana kila mmoja kuchukua jukumu  aliloagizwa.  **
 
Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere
      Eneo la kutokea abiria wanaowasili, alionekana mzungu aliyevaa kofia ambayo ilifunika uso wake kwa kiasi kikubwa. Huyu alishuka akiwa na mkoba  wa begani, huku  akiwa ameshika kitoroli  chenye  sanduku  kubwa la nguo. Alitembea kwa taratibu hadi akafika usawa ambao kuna mwanaume wa makamo mwenye suti nadhifu akiwa amekaa, alipomfikia aliipeleka kofia yake chini zaidi kisha akampita na kutoka kuelekea nje.
     Mtu  yule alimtazama tu   na alipompita alianza kutoka na kumfuata kwa nyuma, mzungu  alifika  kwenye mlango wa gari   kisha akasimama. Muda huohuo   ilisikika kengele maalum na taa za pembeni kuwakaa kuashiria   milango imefunguliwa kwa  rimoti maalum. Alifungua mlango wa pembeni ya dereva akaingia na begi lake, kisha  akaufunga na kuacha kitoroli mahali hapo. Naye a;liyekuwa ameketi kule ndani alifika na kuingia upande wa  dereva.
                           "Brigadia fanya  hima twondoke mahali hapa, kabla hawajajua aliyekuja kunipokea ni nani?", Mzungu yule alisema.
                            "Sawa Alpha usihofu kwa hilo, ila  mbona umekuja na mkoba mkubwa hivyo wakati  hukai kwa muda mrefu huku", Brigadia alismea huku akiwasha  gari.
                             "Mimi ni komandoo   na pia ni mzee wa kazi, fikiri nikija mikono mitupu wakati EASA wananijua fika si ndiyo mwanzo wa kuanza  kufuatiliwa shaka. Wapo airport  nimewaona wa kawaida, pia kuna makachero kadhaa wamepandikizwa na wanafanya kazi mahali hapo. Wakiona na   begi hili hawatodhani kama nimekuja kikazi, watajua ni kutalii ndiyo maana nikabeba mzigo  huo wa nguo maana kama nimekuja kivingine nikibeba hili itakuwa ngumu kutoroka"
                               "Ok nimekuelewa hivi sasa, sasa humo ndani kuna nini?"
                               "Matambara tu   nimeyakunja kama nguo,  tukifika  mbele nitatupa hili begi  halina maana. Mkoba huu  niliyoupakata ndiyo kila  kitu aise"
 
**
 
      Nyumbani kwa Moses majira hayo, Beatrice na mtoto wapo chumbani na sebuleni  yupo Watson na mwenyeji wake wakizungumza. Majukumu waliyepeana ndiyo tayari muda huo wameanza kupatiana  hapo Mzee huyu msaliti wa nchi ambaye anaheshimika kutokana na kuifanyia mengi idara ya usalama wa taifa. Alitaka kujua kile kinachoendelea kuhusu Kaila  hadi akafikia kule, alitaka kumfahamu kwa namna ya kumchimbua maana anaamini Gawaza hakuwa na ubavu wa kumficha chochote   kile kwa jinsi alivyo mshauri kwenye mambo mengi yenye manufaa kwa taifa.
                        "Kijana kwanza nikupe pole sana, nimesikia  rafiki yako amefariki  na mwili wake upo mikononi mwa EASA kiuchunguzi. Mungu amlaze mahala pema Kaila, mpiganaji  na mwanaharakati wa taifa hili", Watson alianza kumchokonoa Moses.
                          "Pole ya nini mzee wangu, Norbert  yupo hai.  Watu waliyofanya kazi ile walichanganya magari,  hawakujua siku ile kulikuwa na magari  mawili ya aina moja kule Karimjee. Wamemuua mtu asiye na hatia, wakimlenga yeye ambaye anaonekana wazi ni chukizo kwao",
                          "Ohoo! Asante Mungu kwa kumuokoa mpiganaji wako, ila kijana wangu nilitaka nikwambie kuwa kesho sitofika stesheni kule Pugu. Mama yangu ni mgonjwa nimepigiwa simu muda si mrefu, kesho nitaelekea Dodoma kwa ndege binafsi kwenda kumwona"
                           "Mr Mbilinyi yaani tumepewa usafiri bora kabisa na unafika huko, kwanini usingetumia hii treni tu hadi huko. Ingawa haiweki kituo hapo Dodoma, ila kwa heshima yako unaweza kushushwa kama tukimshaiwshi mheshimiwa. Huoni ni nafasi hiyo na itaokoa nauli"
                           "Hapana, natakiwa nifike kule saa kumi na mbili. Ili nifanye mipamgo ya kumleta jijini hapa mapema apelekwe hospitali moja kwa moja. Unajua wazi huduma bora ipo hapa jijini kutokana na jinsi sehemu zingine zilivyotupwa kimaendeleo na kutazamwa  Dar tu"
                            "Kwahilo siwezi kukuzua  kwakweli, nafikiri ungeenda tu  kupumzika mzee wangu. Uwahi kuamka  na kufika mapema airport, nikutakie usiku mwema"
                              "Nawe pia kijana wangu", Moses na Watson walipenea mikono halafu mgeni akasindikizwa hadi kwenye maegesho ya nyumbani  hapo ambapo gari la Watson lilikuwepo.
 
**
 
          SAA SITA USIKU,
SEPTEMBA MOSI KUISHA KWA AGOSTI 31
 
      Mitambo  yenye kuongoza kila kitu kilichopangwa nao, ilishawekwa sehemu ya maficho  kwa akina  Huze. Majira hayo  vioo vingi vya tarakilishi vilikuwa  vikitazamana na meza yenye kitambaachi  pamoja na 'keyboard'. Kitini Huze ndiyo alikuwepo  huku wengine wakiwa  wamesimama kutazama  mandhari ya sehemu tofauti ndani ya  treni  ya kisasa ambayo ndiyo  inazinduliwa kwa safari za mbali nchini Tanzania. Mandhari ya ndani ilipendeza haswa, kukiwa ni kutupu huku baadhi ya wanausalama wa idara ya usalama  wa taifa wakionekana  wakihakikisha usalama unakuwepo pasipo wao kubaini ulishakuwa hatarini eneo hilo.
      Kufikia mpango huo ulivyo, kila mmoja  hapo aliendelea kutoa pongezi kwa Besi ambaye alisimama nyuma ya Huze akiwa  wengine wakitazama jinsi  hali ilivyo. Tayari majira hayo Alpha ambaye ni kiongozi wao, alishaweka kiasi kikubwa cha pesa kwenye akaunti yake ya benki kwa kuweza kufanikisha hilo. Kwa jinsi alivyo na   hela nyingi, mwenyewe aliamua kutumia kiasi  kwenye akaunti ya baba yake mzazi kuweza kusaidia matibabu ya mdogo wake. Chuki ile aliyokuwa nayo awali ilimwondoka kutokana na kuzidiwa na furaha kupita kiasi. aliamua kusaidia kabla hajaamua kuondoka nchini na kuelekea mbali baada ya kukamilisha jukumu lake zito.
 
**
     
     ASUBUHI
        Mzee Mluva aliamka na kujiandaa akiwa na kila kitu chake kuhusu safari hiyo ya kwenda Mwanza, mapambazuko yalimkuta akiwa yupo kwenye lango la kuingia ndani kwenye treni. Alishajiandaa kwa ajili ya safari ya kuelekea jijini humo, majira ya saa moja asubuhi ndipo kukafanyika uzinduzi huku mawaziri na sehemu kubwa ya wakubwa wa majeshi wakiwepo eneo la tukio. Rais Zuber alikata utepe kuzindua safari hiyo na akawa wa kwanza kupanda ndani, huku  mawaziri  na viongozi wengine wa taifa la Tanzani wakifuatia kwa nyuma.
         Wananchi nao bila ya kukawia waliingia kwenye mabehewa yao kwa ajili ya safari hiyo,  muda mchache baadaye wanausalama nao walipanda kwa kujichanganya na abiria huku wengine wakiwepo behewa la mbele ambalo lipo jirani na kichwa cha treni  ambapo ndipo  viongozi walikuwepo huko pamoja na waandishi wa habari  ambao walifuatilia kwa kina juu ya tukio hilo linavyoendelea.
         Hatimaye safari  ya Septemba mosi, siku ya  kusherekewa kuundwa kwa   JWTZ. Iliyosubiriwa kwa hamu, ilianza kwa treni hilo kwenda   mwendo mdogo huku milango na vioo vyote vikiwa vimefungwa kwa usalama zaidi. Hatimaye lilichanganya  na kuwa na   mwendokasi mkubwa, wengi waliongea kupitisha muda huku behewa kuu  ndiyo Mheshimiwa akawa anasifia zaidi kwa jinsi safari hiyo ilivyokuwa  nzuri pia ubora  wa vifaa hivyo.
          Wanachi wasiyopanda walibaki wakishuhudia kwenye   runinga zao, namna ambavyo Mheshimiwa ameketi kwenye  behewa la hadhi huku kiyoyozi kikiwa kila mahali. Pia waliweza kuona wananchi wengine wakiwepo kwenye upande wenye ubora zaidi, hakika  lilikuwa ni tukio lenye kufurahisha na kila mmoja akatoa pongezi kwa serikali kuweza kutimiza hilo suala ambalo lilikuwa ni sehemu ya mpango wa muda mrefu. Wabunge ambao hapo awali waliusema vibaya huo mpango wa ujenzi wa reli yenye kasi, walijikuta  wakipanda nao  kutokana na mwaliko maalum waliyopatiwa kwenye safari hiyo.
 
ITAENDELEA


  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4