Friday, 21 March

Ads Right Header

Buy template blogger

Kwanini baadhi ya viongozi wa kidini Washington wamekasirishwa na Trump kutumia Biblia?



Siku chache baada ya Rais Trump kuonekana amesimama mbele ya kanisa la St John Episcopal akiwa ameshikilia bibilia, zaidi ya viongozi 20 wa makanisa kutoka Washington na maeneo yaliyo karibu wamepinga kile alichokifanya.

Kasisi George C Gilbert Senior ambaye ni mmoja wa viongozi hao, aliuambia umati wa watu uliokuwa umekusanyika hapo, kwamba rais alitumia Bibilia "kama chombo cha kuendeleza ajenda yake binafsi".

Kasisi Gilbert amekuwa padri katika kanisa la Holy Trinity United Baptist mjini Washington DC kwa miaka 35. Akizungumza kwa upole na unyenyekevu alielezea kughadhabishwa kwake na kile alichokitaja kuwa tabia "isiyokubalika"

"Huu ni wakati ambao katika historia ya Marekani tunahisi alichokifanya rais wetu, Donald Trump, ni kejeli," alisema.

"Kusimama mbele ya kanisa akiwa ameshikilia Bibilia mkononi wakati hana mazoea ya kuenda [mara kwa mara] kanisani ni kutokuwa mwaminifu na huo ni udanganyifu.

"Hatuwezi kumruhusu afanye hivyo bila kuwaambia watu - na kumfahamisha yeye pia - kwamba hilo halikubaliki. "


Siku ya Jumatatu, rais Trump alitishia kuwapeleka wanajeshi kukabiliana na "makundi ya watu wanaozua vurugu" ambayo anasema yanahujumu maandamano ya amani ya kupinga mauaji ya George Floyd,46, aliyefariki mikononi mwa polisi.

Muda mfupi baada ya kutoa hotuba yake, Rais Trump alitembea mwendo mfupi kutoka Ikulu ya Marekani hadi kanisa la St John's Episcopal - linalojulikana kama kanisa la marais - na kuinua Bibilia mbele ya kamera za wanahabari. Kanisa hilo lilichomwa moto wakati wa maandamano ya siku Jumapili.

Lakini Kasisi Gilbert, na viongozi wengine wa kidini waliompinga, wanahisi hatua ya rais kufika kanisani kwa njia hiyo na kuinua Bibilia, haikuwa sawa na "haikubaliki".

"Alifanya hivyo kupiga picha, na huu sio wakati wa kujionesha"


Muda mfupi baada ya rais Trump kuzuru kanisani, wanahabari waliripoti kuwa vitoa machozi vilitumika kuwatawanya watu waliokuwa wakiandamana kwa amani mbele ya kanisa.

Waandamanaji hao walijumuisha mapadri kadhaa na waumini wa kanisa hilo kutoka dayosisi zingine za mji huo.

Kasisi Gilbert anahisi ni jukumu la waumini wa kanisa hilo kusimama na viongozi wengine wa kidini kupinga hatua ya rais Trump.

"Kama rais wa Marekani, alistahili kutoa hotuba ya kuwatia moyo wananchi kwa kujaribu kuelewa kilichosababisha hali inayoshuhudiwa nchini [ikizingatiwa kuwa] polisi wamekuwa wakiendelea kuwaumiza Wamarekani kwa kuwaua kiholela vijana wadogo, na kuonesha kuwa ''muda umewadia'' kukomesha uovu huo.


Rais Trump hana kanisa maalum analohusishwa nalo lakini uhudhuria ibada ya kanisa mara moja moja kukiwa na hafla maalum.

Amekuwa akitumia ishara na matamshi ya kidini kuwavutia wapiga kura wa Kikristo

Zaidi ya asilimia 75 ya Wainjilisti wazungu walimpigia kura Trump katika uchaguzi wa mwaka 2016, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na kite cha Pew, ikilinganishwa na asilimia tatu tu ya Wamarekani weusi ambao ni wa dhehebu la kiprotestanti.

Kuna baadhi ya wale wanaohisi hali ya Jumatatu ya rais kuzuru kanisa la St John's ni juhudi za rais kuwavutia Wainjilisti wazungu kabla kuelekea uchaguzi mkuu.

Lakini hata wafuasi wa Rais Trump, kama vile mchungaji Burns, wanaounga mkono hatua ya kupiga picha ilikuwa ya kuimarisha msimamo wake wa kisiasa''

"Rais angesifika ikiwa angelitumia nafasi hiyo kuwaomba watu kufanya [maandamano ya amani] na kuwaambia kuwa "Niko na nyinyi, Nitaandamana pamoja na nyinyi, Naelewa kwanini mna ghadhabu."

Hata hivyo Rais Trump ametetea uamuzi weke kwenye Twitter, kwa kuandika: "Mumenielewa vibaya! Ikiwa maandamano ni ya amani, kwanini waandamanaji walichoma Kanisa usiku uliotangulia? Watu walipendezwa na hatua yangu."


  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4