Marekani kufanya mazungumzo mapya na Urusi kuhusu silaha za nyuklia
Marekani imearifu kuwa imekubaliana na Urusi juu ya kuanzisha tena mazungumzo kuhusu udhibiti wa silaha za nyuklia.
Mjumbe maalumu wa Marekani anayeshughulikia masuala ya kupunguza silaha, Marshall Billingslea, amesema kuwa ameafikiana na naibu waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Rjabkov, juu ya tarehe na mahali yatakapofanyika mazungumzo hayo mnamo mwezi huu wa Juni. Billingslea amesema China pia imealikwa kushiriki katika mazungumzo hayo.
Hata hivyo hakutoa maelezo zaidi kuhusu tarehe wala mahali yatakapofanyika mazungmzo hayo. Urusi bado haijathibitisha taarifa hiyo ya mazungumzo.
NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
Previous article
Next article
Leave Comments
Post a Comment