Wednesday, 19 March

Ads Right Header

Buy template blogger

SEPTEMBER 1 SEHEMU YA KUMI NA MOJA.


Why Do Black Women Experience More Pregnancy Loss?

SEPTEMBER 1

SEHEMU YA KUMI NA MOJA.

TULIPOISHIA SEHEMU YA KUMI...

  "Basi kaa hapo utaweza kuona kile  nitakachokifanya,     natumai     tutacheka     wote     kama ilivyokuwa muda si mrefu. Najua wewe ni bingwa wa kucheka, naenda kwa wapumbavu wenzako kisha nitarejea kwako pia usihofu tutacheka  sana. Napenda sana mtu mwenye kufurahi kama wewe"
                         "(Akicheka) Acha kunipiga mikwara Kaila, you are loser"
                         "Hata mimi naona pia"

TUENDELEE...

Majira hayo ofisini kwa Besi, mlango ulifunguliwa kwa  fujo. Aliingia mwanamke huku nyuma kukiwa na katibu muhtasi wake, ujio wake ulionesha wazi  mwanamama huyo aliingia kwa   lazima bila ya ruhusa ya msaidizi wake. Hali hiyo na pia kumwona mahala hapo  mtu huyo, mwenye ofisi alijikuta akisimama wima huku akimtazmaa kwa mshangao.
      Mwanamke yule ambaye ni mtu mzima, alifika na kupiga magoti mbele yake huku  machozi yakimtoka. Hali hiyo ilimshangaza hata binti mwenye kutoa taarifa za wageni wenye kufika  humo, hakujua imekuwaje hadi akafikia kuwa hapo.
                 "Mwanangu naomba msaada wako mdogo wako atakufa yule", Mwanamke huyo aliongea huku akijaribu kugusa miguu ya Besi ila alimkwepa kwa  kurudi nyuma.
                 "Kama kufa tu mwache afe, mimi ndiyo yuleyule uchafu uliyosema marehemu kauacha. Jiulize takataka itaanzaje kukusaidia wewe, mahala pake si jalalani. Katafute isiyokuwa takataka ikusaidie ila siyo mimi, naomba utoke ofisini kwangu kabla sijaita security"
                 "mwanangu nilikosea nisamehe baba, nahitaji msaada wako hivi sasa"
                 "Ulipojifungua     mtoto     si     ndiyo     uliona umemaliza kila kitu, umesahau  hata kesho yako huijui. Basi jeuri zako ndiyo zikulipie  pesa za kumfanyia operesheni, sina  mdogo ambaye ananiita mimi takataka. Uchafu ndugu yake ni uchafu, yeye siyo atawezaje kuwa ndugu yangu, ondokaa!", Besi aliposema hayo alibonyeza kitufe kilichpo ukutani humo  chumbani mwake kisha akaweka mdomo kwenye spike iliyopo jirani na eneo alilobofya.
          Alisema, "Security nawahitaji haraka sana". Muda mchache  baadaye waliingia walinzi wenye sare maalum ambao walimtoa mwanamke yule kinguvu huku akilia. Kwake Besi haikuwa kitu chenye kumuumiza  kila akikumbuka namna ambayo ameishi naye kwa kipindi kirefu tena kwa mateso makubwa mno. Moyo wake ulishaingiwa na giza, haukuona neno msamaha kwake  na kila alipomwona ndiyo hasira zilimzidi zaidi.
                       "Na wewe kaendelee na kazi mtu kama huyo usije ukamruhusu aingie kwa namna yeyote ile", Besi alisema.
                        "Nimemzuia najua huu muda huhitaji mgeni bosi, ila  kaingia kinguvu akisema ni mama yako"
                         "Ita security, nahitaji kuwa peke yangu hivi sasa. Baadaye nitaelekea Pugu kuendelea na kazi  ya kiserikali"
 
**
 
 
       Hali ya gerezani ilikuwa si shwari kwa Gera, muda mfupi alitokea kuwa mtemi wa  gereza lote kwa  wale wanaojifanya wababe. Mwili wake  na jinsi alivyo mbabe ni vitu viwili tofauti, aliweza kuwatuliza  wenye miili ya mazoezi kutokana na mafunzo hatari aliyopatiwa. Ubabe  huo   aliuendelea hadi ikafikia ni mwenye kupiga maaskari kila kukicha, haikupita siku basi askari mmoja akawa ni wa kulazwa  hospitali ya nyumba ya giza. Hilo walimkariri, kila mmoja akimhofia, taarifa zake hatimaye zikafika kwa mkuu wa gereza wa wakati huo. Kamishna James Nkongo, huyu alipokea sifa na namna anavyowapa tabu  maaskari wake.
       Majira ambayo  Besi anamtoa mama yake ndani, alipokea taarifa kupitia kwenye simu ya upepo  afisa mwingine wa magereza anasulubiwa na Gera. Jambo hili liliamsha hasira za Afande Nkongo na kwa  haraka alitoka ofisini kwake akiwa mikono mitupu hakubeba hata rungu, alikimbia kwa haraka kwenda hadi eneo ambalo  mhalifu wao anafanya unyama.
       Alipofika bila kuchelewa alimrukia mateke mawili ambayo yalimpata kifuani akaenda chini, tukio hilo lilifanya ukimya utande humo ndani. Wafungwa wote walimheshimu mno  afande huyo, hakuna ambaye alithubutu kutoa sauti yake. Kila mmoja alitazama kile kinachoendelea kwa kuingia kwake mahala hapo, Gera kwa mara ya kwanza ndipo aliangushwa  chini na alipoinuka alikuta na askari mrefu mwenye mwili wa kimazoezi.
                     "Kila siku unajua kuonea sana vijana wangu, sasa pambana na mimi tuone mimi na wewe nani ataingia hospitali leo. Ukiweza kunifanya nikalazwe naacha kazi hii kuanzia  leo", Afande Nkongo alisema kwa kujiamini.
         Kauli  iliyomfanya Gera amjie kwa kutanguliza teke, mpinzani wake akalikwepa. Akiwa huko kando alipeleka ngumi mfululizo, napo    zikaishia hewani. Alijitahidi kuonesha ujuzi wake kwenye mapigano lakini hakufua dafu, hapo ndipo akabaini amekutana na chupa cha pua. Akabadili  upigani, alidhani angeweza kumpata napo ikawa ni bilabila.
          Zamu yake ya kuanza kushambuliwa ilipofika, alijuta hata  kujaribu kuwa mkorofi humo ndani. Alipigwa kama mtoto mdogo   na  Kamishna Nkongo, mapigo ambayo yalimchakaza hadia akafikia kutokwa  na majeraha mengi mwili wake. Ilifika mahali akawa hawezi kuendelea kupigana kabisa, kweli alikutana na mwamba ilihali amezoea kuchezea mawe.
                       "Nilikwambia ukinipiga mimi naacha kazi, hilo huwezi. Chukueni huyu mtupeni shimo la  kifo, atapasua kokoto akiwa  gizani asione  mwanga wowote kuanzia hii leo. Hakikisha hafi, anatakiwa kubaki hai kwa namna yeyote ile", Afande Nkongo alitoa maelekezo kisha akawagekia     wafungwa          waliyokuwa     wakitazama mpambano. Aliwaambia, "Kila mmoja akaendelee na kazi yake sasa hivi, atakayeleta kiburi nitajua cha  kumfanya mwenyewe. Tulikubaliana  tuishi kwa kiadabu humu, jeuri ya mmoja kitampata kama cha yule. Sipendi kupiga mtu msinilazimishe". Alipomaliza kuongea, aliondoka hapo  huku akitoa kitambaa mfukoni, alijifuta jasho huku akipandisha ngazi kurejea ofisini kwake.
 
**
 
      Kutokana na mtandao mpana ambao  kina Huze wanao, haikuwa jambo la ajabu kwao kuweza kupata taarifa ya kile kinachoendelea. Kwani kukitokea mabadiliko yeyote yale  habari hufikishwa kwa DG wa usalama wa  taifa, na pia makao makuu ya EASA. DG naye alimwamini mno Watson kutokana na ushauri wake kwenye mambo mbalimbali, akamvujishia juu ya habari hiyo.
      Naye hakuiweka moyoni mwake, aliileta moja kwa moja kwa  kaka  wa Gera. Kumpatia taarifa ambayo ilimtia hasira kupitiliza, alitamani hata aende kuvamia kule gerezani na kumtorosha ndugu yake lakini suala hilo haliwezekani.
                 "Nkongo ndiyo anaamua kumtuoa ndugu yangu kwenye shimo la kifo, mahali ambapo si salama kuishi kiumbe wa aina yeyote. Haki ya Mungu nikimtoa huko  ndiyo atajuta, namwambia amalize  familia yake yote", Huze alisema  akiuma meno.
                  "Yaani eneo alilomuweka ni kuna joto, kile chumba kipo chini ya mlima kabisa, kuta  zimejengewa kwenye mwamba. Hakina mwanga na kina joto kupitiliza, kuna tundu la  kupumulia tu, tena akiwa humo amewekewa jiwe kubwa apasue kokoto. Huyu Nkongo ni mnyama  sana", Watson alisema.
                    "Labda     nisiwe     Huze     ninayefahamika, Kamishna  na mke wake ASP watajuta  akitoka kaka yangu. Mshenzi sana, hajui kapata tabu ngapi hadi mimi nipo hapa, leo aje kumtenda tu nasema sikubali"
                     "Kila jambo lina wakati wake, nasi tusubiri wakati wetu tutaweza kumwonesha ni namna gani tuna nguvu.  Sasa hivi  cool down"
 
**
 
       Majira hayo Norbert Kaila alikuwa nyumbani kwa Belinda, alihitaji mno kuonana naye  na wala hakutaka kufika ofisini. Afisa huyu wa jeshi naye alifahamu fika  hakufa kwenye mlipuko ule, hivyo hakushangazwana kuhitajika kwake  kuzungumza naye. Alichukulia ni  jambo la kawaida tu. Aliikacha ofisi na kuwasili hapo, ambapo ni salama kwao kuweka kikao kuliko hata sehemu nyingine yeyote ile.
       Walifikia meza kubwa ya nyumba hiyo, ambao walikaa mkabala. Belinda akiwa na vazi la kazini, huku Kaila akiwa na mavazi yaleyale aliyotoka naye nyumbani kwa Norene.
                  "Nor nipe habari kuna kipi kipya kilichoweza hadi ukaniita huku?", Belnda aliuliza.
                  "Belinda kuna maafisa wawili wa chini yako ndiyo wasaliti wakubwa wa jeshi na sijui  kwanini wanafanya hivyo", Norbert alisema
                    "Are you sure? Hii ni ishu nyingine kabisa"
                    "Hivi nisingekuwa na uhakika ningeweza kukueleza hayo, nimeamua nilifikishe kwako hii ishu wapo maafisa wawili. Mmoja ni kanali mwingine ni one star general"
                    "Kanali na Brigadia, hivi vyeo kuna watu zaidi ya mmoja wanavyo ni ngumu mno kuweza kumpata mhusika mkubwa ni yupi"
                     "Wapo kambi za hapa  jijini, waliyoamua kuvunja kiapo cha utii kisa tamaa zao  za muda mfupi"
                     "Kama     ni     kambi     za     hapa     kweli wanahesabika, jumla kuna makanali kumi na brigadia wapo nane. Wengine wapo nje ya jiji kwenye kamandi kuu ya anga na nchi kavu"
                      " hao kumi na nane, wawili ndiyo wanaongoza huu mchezo wote. Nahitaji ujiibe kwa muda wa ziada huku mimi ninaendelea na  kazi zingine"
                      "Hilo  halina tabu.....enhee! Nimepata wazo Septemba mosi ni siku ambayo maafisa  wote
tutapanda treni kwa ajili ya uzinduzi wake. Siku hiyo ndiyo  nzuri kuhakikisha wote wanajulikana, tutatumia hila"
                       "Mimi sitokuwepo kwenye uzinduzi huo nitakuwa kazini, ila una uhakika wote watapanda?"                         "Wawili tu ndiyo hawatopanda, mmoja atabaki Ngome kiofisi pia kuwasiliana  vikosi vingine kwa ajili ya kuendeleza jukumu la kulinda mipaka ya nchi. Mwingine atatumia  helikopta kuhakikisha kila njia itakayopita treni  ina usalama. Kusitokee ajali ya yeyote, ukumbuke Mheshimiwa yupo ndani pia"    
                   
 
 
                              "Hao wawili ni nani na nani?", Norbert aliuliza
                               "ooh! Sorry ni watatu ambao ni Kanali Seba ambaye anasalia, msemaji mkuu wa jeshi naye vilevile atasalia. Mwingine ni Brigadia Mkunga"
                               "Ok kama ni hao basi  ni kuhakikisha waliyopo mule ndani kwa namna yeyote ile wanajulikana upesi. Tutatumia hila gani kuweza kufanikisha hilo"
                                "Nafikiri     hakuna     hata     mmoja anayeweza kucheza na maisha yake, sasa ni  kuhakikisha muda ambao treni inaenda kila kioo kimefungwa. Baada
ya hapo tutawatisha kama kuna bomu humo, ambalo  halihitaji hewa ya nje linaweza kulipuka"
                                "Tujaribu          hilo,          tukiweza kuwaingiza kwenye  shimo moja kwa moja basi ndiyo  itakuwa mwisho wao"
                                "Vipi ikiwa hawa nje ndiyo wenye kuhusika na mchezo wote huo?"
                                 "Hao ni juu  yako Nor nadhani mimi niachie watakaokuwa ndani ya treni, habari hii nataka niifikishe kwa Afande"
                                  "Hapana si muda wake huo,  sitaki afahamu kama nipo hai kwa hivi sasa. Mwache aendelee kubaki na imani ileile kuwa nimekufa kama ilivyo umma wa  watanzania"
                                   "Ok,     kuna     la     ziada     au  kinachofuatana ni soga"
                                   "Toka lini nikapiga soga kipindi nipo kazini. Nikuage tu niwahi huko niendapo hivi sasa. Kwaheri", Norbert alisema huku akiinuka kwenye kti alichoketi
                                   "Goodluck"
                                   "you  too, usalama kwa Tanzania kwanza mengine yatafuata baadaye"
 
**
 
    Siku  ndiyo zilikuwa zimebaki chache tu, kuweza kufika septemba mosi. Kipindi ambacho  ilitarajiwa vilivyo kushuhudiwa  treni ya kisasa ikianza safari yake ya mara ya kwanza ya masafa marefu tangu reli ya SGR ikamilike.
Kuendelea na maandalizi Mhandisi aliyepangwa kuja kulitazama na kuhakikisha usalama upo,  aliendelea na kazi yake kama kawaida akionesha kujituma.
      Besi ndiyo alichukua jukumu la kuendelea kulikagua na kurekebisha endapo kungeweza na tatizo lolote lile la kuhusu umeme. Pia alitumia njia hiyo kufanya  kazi nyingine aliyotumwa, hakuna ambaye alishtuka juu ya hilo hadi alipohitimisha jukumu lake ambalo ameahidiwa mamilioni ya fedha.
        Laiti kama serikali ingelimjua huyu mtu na uhalisia wake, basi wasingelimpa   jukumu hilo kisa tu ana utaalamu wa umeme. Fisi  hakabidhiwi  bucha alilinde  pasipo kutia hasara yeyote, hilo jambo  hakuna aliyeweza kumaizi hadi alipokamilisha na kulipwa ujira mkubwa akarejea walipo wenzake. Ni zaidi ya kosa kubwa kwa serikali, ambalo wamelifanya bila ya wao kujijua.
       Huko aliwasimulia kila kitu juu ya kinachoendelea, pongezi nyingi alipatiwa na pia kuongezwa malipo zaidi kuliko yale aliyopewa na serikali kwa kazi aliyoifanya. Watson aliyehakikisha Besi anawepo kwenye hila hiyo, alitoa  donge noo ambalo kijana huyu hakuwahi kulipwa kabla ya siku hiyo. Muamala wa fedha uliingia kwenye  simu kuonesha pesa hizo zimepelekwa kwenye akaunti yake, jioni ya siku hiyo ilibidi waweke sherehe kwa ajili ya kufurahia jambo hilo ambalo walilisuka kwa muda mrefu  kuja kufikia tamati.
                   "Hivi sasa hakuna  injinia hatari kwenye sehemu yeyote ila ya nchi hii, wewe ndiyo mkubwa wao
Besi. Pesa hizo bado tu Mkuu  atakuongeza subiri sasa hivi tukimpa taarifa, hutojuta kuwa nasi", Watson alisema  usoni akiwa na tabasamu mwanana.
                   "Besi wewe ni kichwa aisee, hii project yako ambayo umetumia muda mrefu kuweza kuiandaa  basi tambua hakuna kiumbe ambaye anaweza kuifikia. Sijawahi kuona kitu kama hicho tangu niingie kwenye huu mchezo. Wewe ni  genius",  Huze naye alimpongeza huku akigonganisha  mkono naye.
                    "Wote mnajua jinsi nilivyokuwa na hasira  na serikali hii, mateso yote ya ajira na elimu  kubwa kisomo changu cha maana. Sifa kedekede nilizopewa nikiwa  field walitegemea niitumie elimu yangu kinamna gani, yaani unashuhudia mtu ambaye umemzidi kila kigezo anapata ajira ila mimi niliye na ufaulu mzuri sijafikia hapo walipo. Fools all of them, sijaona maana ya elimu yao zaidi ya kuiona hii mliyoniongeza nyinyi. Watajuta majuma mawili mbali, hiyo sikukuu  ya majeshi itakwua ni kilio kwao na si kingine", Besi alisema huku akigonganisha  bilauri na Watson.
                     "Rais ndani, makamu wake ndani, mawaziri ndani, mkuu  wa majeshi ndani, mnadhimu mkuu ndani, IGP ndani, DIGP ndani, CG wa  magereza ndani, DG wa TISS ndani na  makomandoo  ndani. Shetani ataizidi dua  zao za ufunguzi nguvu", Huze aliongea.
                       "Umewasahau     na     wananchi     wenye kiherehere cha kwenda Mwanza na Kigoma kwa muda mfupi nao  itawakuta ileile. Halafu kitu chetu kilaini tunakipata, mnaonaje kwenye mpango huu watuongeze na dhahbu zote zitakazotoka Geita kusafirishwa  zije kwetu", Watson alisema.
                       "Hilo ni wazo zuri yaani tukitoka hapa ni mwendo wa kuwa  billionea, tutawaachia nchi yao na hasara ambayo hawajawahi kuipata", Huze alisema.
    Waliendelea kunywa  na kufurahi, kwa kukamilisha sehemu ya mpango wao ambayo itahitaji utimizwaji tu waweze kufikia kilele cha mafanikio. Watu hawa walikuwa tayari kwa lolote, ilimradi tu wafikie malengo yao waliyoyaweka.

ITAENDELEA



  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4