Monday, 17 March

Ads Right Header

Buy template blogger

SEPTEMBER 1 SEHEMU YA KUMI NA TANO.



Why Do Black Women Experience More Pregnancy Loss?ILIPOISHIA JANA.

Mheshimiwa          tafadhali     msikilize Belinda, tuachie  hili suala lipo kwetu hivi sasa. Mimi, CGP, IGP na DG tutashughulika. Nakuomba uwe na kifua cha kutunza siri na pia  uwe na subira, tupo kwa ajili ya roho za maelfu ya watanzania waliyopo humu ambao ni jukumu letu kuhakikisha hawadhuriki", Jenerali Marwa alisema, Rais Zuber hakuwa  na  hiyana alitoka mwenyewe nje ya  chumba hicho cha dereva wa treni. Alirejea kule walipo viongozi wengine wa kisiasa na kiserikali, alikaa kama vile hakuwa akijua kinachoendelea humo na  hata alivaa  tabasamu la bandia usoni mwake.

ENDELEA NAYO.

**
 
       Mzee wa kazi aliamua kuifanya dhima kinamna yake,  kutokana na muda wa masaa 48 waliyopewa ikimaanisha Septemba tatu ndiyo mwisho wa kuishi kila mmoja aliyepo ndani ya chombo kile. Aliamua kuingia kwenye msako wake, Besi alihitajika kupatikana kwa gharama zozote  zile. Akiwa kwenye mwendo wa kasi alifika nyumbani kwa mshukiwa wake, ulinzi  ulikuwa mkali mno  kukiwa na walinzi wenye sare sawa na wale waliyomshambulia kule darajani.
      Norbert akiwa na silaha zake kiunoni, aliegesha gari kwenye miti  mingi kisha akashuka akiwa amevaa  glovu nyeusi mkononi. Mbali na  bastola mbili, alichukua visu   vinne vikali na aliweka kiunoni vyote vikiwa kwenye ala zake. Uso wake haukuwa na mzaha kila alipofikiria ni roho za watu  waliyopo kwenye treni ile.
      Uzio wa nyumba ya Besi aliuruka kwa  sarakasi moja  na alipotua ndani alibimbrika chinii. Kitendo cha  yeye kuingia walinzi wawili waliyopo jirani na uzio walimwona, ila aliwahi kuwamaliza kwa  kumpiga mmoja karate mbili za haraka. Ya kwanza ikipangua silaha na nyingne ikimpiga  shingoni akapoteza fahamu. Aliyesalia alipojaribu kuinua silaha kwa  hima, alikutana na pigo la judo ambalo lilimpeleka chini huku akiwa amepigwa kabali  ya miguu. Alibanwa hivyo hadi alipotulia ndipo akaachiwa, Kaila alijilaza vilevile pamoja  na kuwamaliza  huku akitalii mazingira  ya hapo ndani.
        Upande wa  getini aliona walinzi wawili wakiwa hawajui kinachoendelea, upande mwingine kuelekea nyuma ya nyumba aliona ni kweupe hakuna kiumbe yeyote. Bila  kuchelewa alitoa bastola zake mbili  kiunoni. Aliwalenga  kichwani kila mmoja, kutokuwa mlio kulimpa wasaa wa kutenda jambo la upesi    bila  kugundulika. Aliwalamba risasi za kichwani kila mmoja, tendo  hilo alipolifanya alichukua  bunduki moja ya walinzi wale kisha akapiga sarakasi upesi  na alipotua alimbimbrika hadi akafikia kwenye ukuta wa  nyumba akajibanza. Tukio alijua wazi kungejitokeza walinzi wenye kutazama eneo la langoni  kama wapo
        Kweli  kulisikika vishindo vikija hapo, Norbert alijiandaa vyema kwa kuweka bastola zake kiunoni kisha akachukua  bunduki ya kivita aliyoitwaa humo ndani. Walindaji waliyotoka huko  nyuma walifika wakiwa  hawana mahesabu yeyote, kitendo cha wao kujitokeza aliamua kuchungulia tu akawamiminia risasi. Wanne kati yao wakaanguka papo hapo, wawili wakasalia wakawa wakimimina risasi  upande  aliyopo. Norbert alirudi nyuma kwa kasi, hadi usawa ambao  kuna  bomba la kutolea  harufu chooni usawa  wa madirisha mdogo ya choo. Bila kukawia aliruka juu  akashika kingoa  za    madirisha madogo, alijivuta juu kwa haraka akafika batini ambapo alitulia kimya kama vile hayupo.   
 
     Loh! Magadi wale walikosea hesabu haswa, walikuja upande uleule kichwa kichwa  huku wakimimina risasi wakidhani watampata mtu wao. Hadi walipofika  sehemu ile hakumkuta, wakiwa wanashangaa ndipo mwenzao akawamaliza kwa pamoja akiwa amejishikiza kwenye paa la nyumba hiyo. 
    Norbert alipoteketeza sehemu kubwa ya  walindaji, alishuka huko juu alipokuwa huku silaha aliyoichukua humo ikiwa ipo tayari kwa lolote. Alitembea hadi mlango wa mbele wa jengo hilo, huo alijaribu kuufungua ila haukutii amri. Hii  ni ishara tosha ya kuwa humo ndani hakuna kiumbe wa aina yeyote ile au yupo hajatoka nje. Aliamua kuufungua kwa  funguo malaya, akaingia ndani  ambapo alitokea kwenye sebule ya kisasa kulipokuwa kuna picha za Besi zikiwa ukutani.
    Upendezaji wa kikaribisha wageni kwake haikuwa na maana, zaidi ya kupekua ndani humo kumtafuta mhusika lakini hakukuwa na mtu. Pia  hakuona cha maana kilichopo ambacho kingeweza kumsaidia walau kumpata mhusika wake. 
     Aliamua kutoka nje hadi alipo  mlinzi yule ambaye alimzimisha  tu, alimfikia na kumtoa kila kitu cha hatari mwilini mwake kisha akamburuza hadi eneo ambalo kuna  bomba la maji linalotumika kumwagilia maua  yaliyopo bustanini humo ndani. Norbert alimwinamisha kwenye koki ya maji, alifungua   na kumlowanisha kichwa chake hadi pale alipozinduka na kuanza kuleta kukurukakara zake. Kufikia hapo alimwondoa bombani kwa nguvu kisha akamsukuma kwenye majani,  mlinzi  yule aliangukia  chali na alipoinua uso kumtazama aliyemfanyia hivyo alikutana na mdomo wa bunduki.
                    "Mwenye nyumba yupo wapi?", Aliulizwa swali  na kisha risasi   takribani tatu zikapigwa jirani na miguu, haikumpata hata moja ila uoga aliyokuwa nao alishtuka haswa na kuanza kusota kurudi  nyuma.
                     "Siulizi swali mara mbili, unanipotezea muda", Alipotoa kauli hiyo alimtandika risasi moja ya  gotini na kupelekea damu zianze kumvuja, mlinzi  yule aliona hakuna ulazima wa kuficha   tena kwa jinsi alivyojeruhiwa na pia adui yake bado ana silaha. Alibaki kimya huku akiendelea kujitazama nguo yake ya ndani baada ya kuvuliwa  koti la juu, hapo ndipo alijiona hana ujanja na amefika pabaya.
                       "Inaonekana nyinyi ni zaidi ya walinzi ndiyo maana hadi kola zenu zinawekwa sumu mlambe mkizidiwa. Si kampuni ya ulinzi ya kawaida, nyinyi. Sikia wewe usinipotezee muda hapa kama ni hiyo nguo tayari nimekuvua huna namna ya kulamba sumu ufe",  Kaila aliongea huku akimlenga na mdomo wa mdomo wa bunduki kwenye goti jingine.
                      "Mkuu Besi  hayupo hapa, anaondoka usiku wa leo kuelekea Komoro. Hapa kahama na kila kitu chake"
                       "Swali     nililokuuliza     ni     yupo     wapi, sijakuuliza anaenda wapi"
                        "Sijui hivi sasa alipo, naomba usiniue ninahitajika na familia yangu"
                        "Ili ukatoe taarifa kuwa umevamiwa  wazidi kujificha nisiwafikie siyo, umechelewa", Norbert a;liposema maneno hayo alimmiminia risasi za kifuani na   kumpiga moja  ya  kichwani.
      Alipotimiza hayo aliamua kwenda hadi kwenye kibanda cha ulinzi  kwenye  nyumba hiyo, hakukubali kuwa amewakosa hivihivi wabaya wa nchi wakiwa wameweka masharti magumu kutimizika. Huko alikutana na kitabu  cha wageni, pia kukiwa na simu ya mezani pamoja na kitabu kingine chenye namba za  simu. Hapo alijikuta akiachia  tabasamu, kwa kuona amepata namna ya kuanzia, kuwepo kwa kitu kama hicho kwake ni ushindi  tosha  ambao alihitaji kutafuta namna ya kuupata tu na si vinginevyo.
Mawasiliano ya 'fax' hatimaye  yalitumika, yalitoka kwenye treni hadi ofisi ya mkuu wa gereza la nyumba ya giza. Taarifa ya kile kilichowakuta  wakuu wa nchi pamoja na wa kijeshi, zilifika kwa Kamishna Nkongo. Karatasi yenye kutoa maelezo hayo aliipata kupitia   mashine hiyo, aliyasoma na kuelewa sehemu ya masharti yaliyopo ili watu wote waweze kukombolewa kwa haraka.
        Hayo ndiyo mambo magumu kwake, yaani kumwachia mtu  hatari kama yule  pamoja na kupatiwa  chombo  cha kutorokea kama ikiidhinishwa juu ya jmbo  hilo. Kwake ni mtihani haswa, akifikiria  jinsi alivyomfungia kiumbe hatari mule ndani. Hali ilivyo aliona ingekuwa ni mbaya zaidi kama angeendelea kumuweka kwenye   chumba   chenye mateso. Aliamuru atolewe na kurejeshwa    magereza ya kawaida, huku akitafakari itakuwaje kama ingetolewa amri kama hiyo huko EASA.
      Ofisini muda huo  alikuwepo mkewe wake ambaye pia ni askari, tena akiwa  mmoja wa wasaidizi mahala hapo.
Habari hiyo naye aliisikia akaone ugumu wake, kama ingeweza kutimizwa kwa kufuata matakwa  ya magaidi.
                     "Unajua huyu mtu ni gaidi kabisa fikiria  tukimwacha awe  huru  nini itakuwa kwa nchi hii. Tukumbuke hakukuwahi  kuwa  na makubaliano yenye usawa kati ya serikali na magaidi, maadui hawakubaliani  lazima  kutakuwa na usaliti", Mkewe alisema.
                     "Hilo suala nalielewa Teddy lakini fikiri kwa umakini itakuwaje sasa, wakuu ndiyo waamuzi wake yaani hapa   huyu mjinga nitamani hata nimwangamize unajua baba yupo kwenye treni ile ni hatari hii. Hii  fax katuma yeye hivi sasa", CP Nkongo alisema.
                     "Hebu tuwe na subira na suala  hili tulifikisha kwa wenzetu wote, huyu  gaidi hastahiki hata kuwepo humu. Hukumu yake ni kifo tu na si kingine"
                     "Nahitaji tukae kikao cha dharura na wengine mahala hapa"
 
**
 
      Baada ya kufanikiwa kutuma pesa kwenye  akanti ya baba yake, alisahau kumkumbusha juu  ya msaada aliyowapatia. Ndipo akiwa na wenzake kwenye maficho yao aliamua  kupiga simu na kumpa taarifa ya kumtuma pesa. Besi hapo ndipo akajikuta akipokea habari mbaya, mzazi wake  naye yupo ndani ya treni ileile ambayo kaweka bomu kwa ajili ya kulipua maelfu ya raia wa nchi ya Tanzania wakiwemo viongozi wa nchi na hata wakuu wa majeshi.
     Loh! Kumfanyia mtu ubaya ni kitu chepesi sana ila ukikurudia  wewe ni jambo jingine zito sana kukabilika. Besi alijikuta  akijiwa na uchungu moyoni mwake, anaenda kumwangamiza mzazi wake aliyemlea kwa muda mrefu kisa tu tamaa zake za muda mfupi. Kama ni kutafuta pesa ila si kukaribia   kutoa uhai wa wengine, alijikuta akieleza hilo kwa  Watson ambaye alimshangaa sana akiona anaweza kuwasaliti ndani ya muda wowote ule. 
      Alidhani mzee huyo ndiye ambaye angeweza kumsaidia kwa jinsi alivyompigania hadi akawa hapo. Kumbe  anampa habari mtu mwenye roho ya paka, ambaye aliamua  kumpa pole kinafiki na kuahidi kumsaidia tu huku kichwani akiwa na lake. Alipofanikiwa kumweleza hilo simu iliingia  kupewa taarifa ambayo ilifanya wengi washangilie mahala hapo. Eti Norbert Kaila  ameshikwa nyumbani kwa Besi, baada ya kupigwa kitako cha bunduki akapoteza fahamu.
                   "Habari njema hii jamani, aliingia kikondoo tu akakutana na wazee wa kazi. Nasikia aliruka ukuta ile katua ndiyo jamaa akamuwahi na kitako cha  bunduki. Sasa huyu nataka akauawe mara moja", Huze alisema kwa furaha.
                    "Besi  kwakuwa wewe hapa hauna  kazi nyingine, basi hili jukumu nakwachia wewe,  nenda  kamhoji huyo mjinga kama ana chochote cha kusema utuletee tumia mbinu za kijasusi kumbana asema. Akisema mmalize, asiposema asipone  vilevile", Watson alisema, huku akimgeukia Huze akamuuliza, "kuna habari yeyote ile kutoka kwa kina Kanali na Brigadia?"
                     "Hadi sasa sijawapata na simu zao  hazipo hewani, nahisi  ndiyo wapo kazini kumbukeni walisema  wakiingia shughulini hawatoshika simu", Huze alijibu, muda huo tayari Besi alishatoka kwenda alipoambiwa akiwaacha wenyewe humo  ndani
                      "Hivi Watson kwanini hii kazi kwa haraka umempa Besi, kama itatokea tatizo lolote hapa la kimitambo nani wa kuja kulitatua. Nimekaa kimya tu sikupinga, lakini nadhani kuna jingine umeliwaza", Alpha alisema.
                       "He is stupid, anaendeshwa na  emotion kuliko akili. Kwenye treni yupo baba yake mule kajua hilo, eti ananiambia nimsaidie aokoke. Maana yake tusilipue  bomu kisa kuna mzazi wake, unafikiri ana umuhimu gani huyu. Huze toa taarifa kwa walinzi akifika huko wammalize yeye na Kaila hakuna namna, nimempeleka huko ili wakamuue tu", Watson alisema.
                         "Wooow!     Umecheza     kama     pele  Watson, angeweza kuwa kikwazo  kwetu huyu tena ningemwachia aweke password yeye angeweza hata kuirukia system ya bomu kwa kutumia  PC nyingine atufelishe", Huze alisema huku akiinua mkonga wa simu akabonyeza namba kadhaa kisha akaweka sikioni, alisubiri simu ilipoita hadi ikapokelewa. Aliongea, "Guard sikilizeni kwa umakini  Besi anakuja  yupo njiani tumempa kazi moja tu ya kumwangamiza Kaila, ila haikuwa lengo hilo bali tumemleta huko mumwangamize. Hakikisheni Kaila na Besi wote kwa pamoja wanaangamia hii amri"
                          "Watson wewe una akili sana, huyu mjinga umemuweza haswa kwa kitu hicho ulichokifanya", Alpha alisema.
                          "Huyu ni magugu  hivi sasa, mwache akakutane na mafuta ya taa  huko, afe  bila hata ya kuwashiwa kibiriti", Watson alijitapa.
 
**
 
     Besi akiwa  yupo  ndani ya gari lake aliendesha ka kasi kubwa, akiwa hana lengo la  kummaliza Kaila isipokuwa ni kuweka mkakati mwingine.  Tayari alishafanya kitu ambacho ni pigo  kwa akina Huze, wao  hawakujua waliona ni wanaenda kumaliza mchezo. Alifanikiwa kufika hadi nyumbani kwake, akafunguliwa  geti akaingiza gari ambapo alisimamia eneo la jirani na kibanda  cha mlinzi. Alishuka huku geti likijifunga lenye kwa mtambo maalum, alipiga hatua zake ndefu akielekea upande wa mlango wa banda hilo, huko alikutana na ukimya ambao siyo wa kawaida.
     Ilimbidi afungue na alipofanya hivyo, alikutana uso kwa uso na mdomo wa bastola  yenye kiwambo cha kuzuia   sauti. Hakutarajia suala hilo, akataka kufanya  ujanja, alijikuta akitulia baada ya  mkono wa pili  kuongezwa ukiwa na silaha vilevile. Mwenyewe aliweka mikono juu huku akirudi nyuma na Kaila akaonekana akitoka kwenye kibanda  cha ulinzi.
                  "Umekuja kumuua Kaila  siyo, hongera sana   kwa mtego wangu umejileta mwenyewe mahala hapa", Norbert alisema.
                    "No! No! Kaila sipo kwa lengo hilo, baba yangu yupo kwenye treni Kaila. Wale wajinga wamejua hilo ndiyo maana wakaniagiza haya ili  walinzi wa huku waje kuniua. Nimesikia mipango yote baada ya kutoka ndani ya control room, nikabana mlangoni. Sipo kwa lanego hilo, nahitaji  mzazi wangu aokoke", Besi alisema.
                     "Kama isingekuwa mzazi wako kuwa kule ungefanyaje? Yaani upo radhi kabisa kupoteza maisha ya watanzania wengine kisa uwepo kwenye maisha mazuri"
                      "Kaila ondoa silaha usoni kwa Benjamin,  huyo si adui yetu kwa sasa ameweza kuwa msaada kwetu", Sauti nyingine ilisikika na hatimaye akajitokeza mtu aliyevaa gwanda la kijeshi ambalo limeweka weusi kwa uchafu.
                        "Luteni Mfuruki  ni wewe kweli?", Norbert aliuliza akiwa  haamini.
                        "Ndiyo mimi, huyu bwana  baada ya kujua kama  yupo upande mbaya wenye kutaka kutoa uhai wake. Aliamua moja kwa moja kuja hadi tulipofungiwa baada ya kutekwa, hivi ninavyoongea ameikomboa bomb squad yote na amekuja nayo kwenye gari alilofika nalo. Anatakiwa atusaide hivi sasa", Luteni Mfuruki alisema, Kail alishusha silaha  chini kisha akamtazama Besi.
                         "Benjamin  umefanya kosa kubwa pia ingawa umeweza kuwakomboa maafisa hawa wote, wakijua kama umeondoka nao basi jua watahamisha kambi haraka iwezekanavyo. Maana unajua walipo na walituma kukuua,  mpango wao umefeli kuchomeshwa ndiyo kunafuata", Norbert alilalamika.
                         "Unafikiri ningefanyaje Norbert,  hawa wangeuawa wote leo leo. Alpha kafika kwa ajili ya kuondoka na  timu yake na kuua wote hawa", Besi alisema.
                          "Alpha ndiyo nani?"
                          "Mkufunzi wa zamani wa Cuba kwenye kikosi cha komadnoo, anaitwa Timothy. Yeye ndiyo alifadhili hadi nikaweza kupata ujuzi wote huu niliyonao, ni mtu hatari sana huyo", Besi alieleza, hapo ndipo Norbert akajua  mtu ambaye walimwamini na kufanya naye kikao juu ya  kutafutwa kina Huze  ndiye anayewatuma kufanya kazi hizo. Doh! Waliuza mpango wote kwa adui bila ya kujijua, aliweka mkono usoni huku  akijuta kwa  maafisa wa shirika lao kufanya yale. Norbert alisema, "Ooh! No! No! No! Huyu mtu    tumeshauza  sehemu ya siri zetu, kikao cha kuwatafuta hao watu alihusika".
                         "Jamani hapa  cha maana ni kujua jinsi gani tunaweza kuwakomboa  waliyopo kule hebu hayo mengine tuache. Msifikiri kuna makubaliano  na ambayo yatawekwa, jueni hata masharti yalitolewa yakitimizwa treni inalipuliwa. Yasipitimizwa ni vilevile. Muhimu ni kutegua hilo bomu kuliko kitu kingine, tusiangalie masharti yao. Mimi ndiye niliyetumia miezi  kuliunda lile bomu,  password ameweka Huze mwenyewe siwezi kulitegua  pia. Haliteguliwi kwa nyaya zaidi ya password tu na si kingine, najuta kutumiwa na washenzi wale", Besi alisema.
                          "Sasa sikilizeni kwa umakini, mimi nimepata wazo hivi saa. Mfuruki na Benjamin nyinyi nendeni kambini mjue mtalitatua namna gani. Mimi ninaelekea makao yangu ya kikazi hivi sasa, mjigawe hakikisheni wengine wanafika kule kwenye makao ya kina Huze tubahatishe kama wapo au lah. Tusidharau kitu, kukiwa na jipya mimi nitajua ni namna gani tunaweza kulitimiza", Kaila alisema huku akitoka kwa haraka, wengine nao walimfuata kwa nyuma huku wakiwa hima kuokoa  maisha ya wasiyo na hatia.

ITAENDELEA


  NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WENYE ELIMU KUANZIA DARASA LA SABA ,KIDATO CHA NNE,CERTIFICATE,DIPLOMA,DEGREE NA KUENDELEA ZIPATE KUPITIA AJIRA FORUM APP 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Leave Comments

Post a Comment

Ads Post 4